Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, June 6, 2010

Mikel kutocheza Kombe la Dunia, majeruhi

Kukosekana kwa Obi Mikel ni pigo kwa safu ya kiungo ya Nigeria.

Kiungo wa timu ya taifa ya Nigeria, John Mikel Obi, ametangaza kujitoa katika michuano ya Kombe la Dunia 2010 huko Afrika Kusini kutokana na majeraha ya goti.

Mikel anaungana na nyota wengine wa Chelsea, Michael Essien na Michael Ballack ambao watakosa michuano hiyo mikubwa kutokana na majeraha, pia kuna wasi wasi kuwa Didier Drogba naye huenda asicheze.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, alifanyiwa upasuaji wa goti mwezi Mei, lakini amesema bado hajisikii kuwa amepona kikamilifu kiasi cha kucheza katika Kombe la Dunia.

"Tumemwondoa Mikel kutoka kikosi chetu baada ya kueleza kuwa asingependa kuhatarisha uchezaji wake," msemaji wa timu ya Nigeria alieleza.

Nafasi yake Obi Mikel itajazwa na Brown Ideye, mshambuliaji kutoka klabu ya Sochaux ya Ufaransa, ambaye hajawahi kuchezea timu ya taifa ya Nigeria.

No comments :

Post a Comment