Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, June 6, 2010

RAIS WA RBP KUIPELEKA TWIGA STARS KAMBINI MAREKANI!!

Rais wa RBP OIL & Industrial Technology Tanzania Limited Rahma Al Kharoos akiongea na waandishi wa habari leo kwenye Hoteli ya Movenpick jijini Dar es salaam kulia ni Meneja Huduma wa kampuni hiyo Ibrahim Khatrush


Rais wa kapuni ya mafuta ya RBP Oil & Industrial Technology Tanzania Limited Rahma Al Kharoos ametangaza ziara ya timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars kwnda nchini Marekani kwa mafunzo mbalimbali wiki ya kwanza ya mwezi Agosti.

Akizungumza kwenye mkutano na wandishi wa habari katika hoteli ya Movenpick jijini Dar es salaam Rais huyo amesema anaamini kuwa ziara hiyo itakuwa ni chachu ya mafanikio ya timu hiyo wakati itakapokwenda kucheza katika fainali za kombe la mataifa ya afrika kwa wanawake mwezi septemba nchini Afrika Kusini.

Amesema akiwa kama mlezi na mdhamini wa Twiga Stars na kwa kushirikiana na wenyeji wa ziara hiyo huko Marekani ambao ni taasisi ya FREEDOM WASHINGTON wamejipanga kuhakikisha ziara hiyo inakuwa ni ya mafanikio hasa ukizingatia kwamba timu ya Twiga Stars imeweka historia kwa nchi yetu kushiriki kwa mara ya kwanza katika mashindano hayo makubwa ya mpira wa miguu kwa wanawake.

Ameongeza kuwa Twiga Stars ikiwa Merekani itacheza michezo minne wa kwanza utakuwa ni wa kuchangia timu hiyo (Charity) ambapo watu mbalimbali watachangia timu yetu ili iweze kujiandaa vyema na mashindano hayo.

Jana Twiga Stars ilifanikiwa kukata tiketi ya kucheza fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa wanawake nchini Afrika kusini ambazo zitafanyika mwezi septemba mwaka huu baada ya kutoka sale ya magoli 3-3 na timu ya Eritrea.
Naomba wadau, wapenzi wa soka la wanawake kuiunga mkono timu hii ambayo imeleleta sifa na heshima taifa la TANZANIA kwa kupata nafasi hiyo ya kushiriki michuano mikubwa zaidi baraNI Afrika kwa wanawake. Naamini kuwa sasa milango ya wachezaji wanawake kucheza soka la kulipwa nje itatimia.

No comments :

Post a Comment