Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, October 12, 2010

WIZARA YA HABARI UTAMADUNI NA MICHEZO YAAGIZA TFF KUANZIA SAS A KUTUMIA BRASS BAND WAKATI WA MECHI ZA KIMATAIFA NA SI VINGINEVYO

Katikati ni katibu mkuu wa wizara ya habari utamaduni na michezo SETTI KAMHANDA kulia kwake ni mkurugenzi wa idara ya michezo THADEO na kushoto ni mkurugenzi wa MAELEZO CLEMENT MSHANA
Mkurngenzi wa idara ya michezo LEONARD THADEO akiju swali kwa waandishi wa habari
Katibu mkuu wa wizara ya habari utamaduni na michezo SETTI KAMHANDA akiwa na mkurugenzi wa idara ya michezo LEONARD THADEO .
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, GEROGE MKUCHIKA, ameliangiza shirikisho la mpira wa miguu nchini TFF kuhakikisha kuanzia sasa nyimbo za taifa katika michezo yeyote ya kimataifa zinapigwa na BRASS BAND, ili kuepuke aibu na fedheha kama zile zilizotokea juzi kwenye uwanja wa taifa wakati wa mechi kati ya TAIFA STARS na Morocco.

Akizungumza kwa niamba ya waziri Mkuchika,katibu mkuu wa Wizara Habari, Utamaduni na Michezo SETTI KAMHANDA amesema kitendo cha kutopingwa nyimbo za taifa kilichotokea siku ya jumamosi kilisababisha adha kubwa kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, JAKAYA KIKWETE,mashabiki waliohudhuria mchezo huo na wananchi.

KAMHANDA ameongeza kwamba WAZIRI MKUCHIKA ameliangiza shirikisho la soka nchini TFF, kuhakikisha linachukua hatua kali dhidi wale wote waliohusika kulitia aibu taifa kwa kushindwa kuwezesha kupingwa nyimbo za taifa wakati wa mchezo kati ya TAIFA STARS na Morocco

Wakati Mkuchika akitoa agizi hilo, tayari shirikisho la soka nchini TFF, kupitia kwa RAIS wake LEODGER TENGA tayai limeshamsimamaisha kazi Afisa habari wake FLORIAN KAIJAGE kwa uzembe huo na kwamba atisaidia tume itakayoundwa kulichnugza sakata hilo.

Katika mchezo huo kundi D, uliochezwa kwenye uwanja taifa jijini DSM STARS ilifungwa bao moja kwa bila na Morocco.

MSANII SALIF KEITA KUTOKA MALI KUTUMBUIZA MOVENPICK DSM JUMATANO KESHO

Msanii KEITA akisalimiana na kiongozi kutoka chama cha albino nchini wakti wa mkutano na waandishi wa habari
msanii SALIF KEITA
Msanii SALIF KEITA katika akiongea na waandishi kulia kwake ni meneja masoko kutoka banki ya stanbic singano

SALIF KEITA kutoka MALI kutumbuiza Dar

Mtuzi na Mwimbaji wa Mziki kutoka MALI, SALIF KEITA, maarufu kama,(GOLDEN VOICE OF AFRICA) anatarajiwa kukonga nyoyo za mashabiki wa mziki atakapopanda jukwaani kutupuiza jijini DSM hiyo kesho .

MENEJA MASOKO wa BANKI ya STANBIC ambao ndio wadhamini wakuu wa ziara ya mwanamziki huyo, ABDALLAH SINGANO amesema pamoja na kutumbiza kwa nyimbo mbalimbali pia ataimba nyimbo zinazohusu nyimbo zinazopinga unyanyasaji na mauja ya Albino nchini na Afrika kwa ujumla.

KEITA ambaye pia ni Albino, amesema binaandanu wote ni sawa,wameubwa kwa rangi na mabakila mbalimbali ili wapate kujuana,na kuzaliwa Albino hayo ni majaliwa ya mungu na si changuo la wao Albino kwa hivyo hawabanguliwe wala kuuawa.

Katika onyesho hilo litakalotubuizwa na SALIF KEITA,pia atazidikizwa na mwanamuziki wa tanzania mwanadada KEISHA.

KUZIONA SIMBA NA YANGA ELFU 30 KATIKA UWANJA WA CCM KIRUMBA MWANZA


Kaimu katibu mkuu wa TFF SUNDAY KAYUNI ametanganza viingirio katika mchezo wa watani wa jadi simba na yanga mchezo utakaofanyika jumamosi ijayo katika uwanja wa ccm kiruma mkoani MWANZA.
AMESEMA KIINGILIO KATIKA MCHEZO HUO NI, MZUNGUKO ELFU TANO WAKATI VIP SHILINGI ELFU THELATHINI.
Wakati huo huo KAYUNI amesema msafara wa viongozi watatu wa TFF wameondoka leo kwenda CAIRO MISRI kuhudhuria mkutano wa shirikisho la soka Afrika, CAF wa kutadhimini michuano ya fainali za kombe la mataifa Afrika CAN yaliyofanyika Angola mwaka 2008.

Viongozia waliondoka ni rais wa TFF leodiger tenga,kaimu katibu mkuu wa TFF Sunday kayuni na kocha wa timu ya taifa JAN PAULSEN.

No comments :

Post a Comment