Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, June 18, 2013

'NYOTA NJEMA' YA SALMA SEGERE YAANZA KUTESA






Na Elizabeth John

MWANADADA anayetamba katika tasnia ya muziki wa Taarabu nchini, Salma Swed ‘Salma Segere’ ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Nyota Njema’ ambao umeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Mbali na kibao hicho mwanadada huyo alishawahi kutamba katika vibao vya Segere, Lindima, Alongore na vinginevyo ambavyo vimeimbwa na kundi la muziki huo la Wazazi Culture Troup ‘Segere Original’.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Salma Segere alisema anamshukuru mungu kazi hiyo inafanya vizuri katika tasnia ya muziki huo ikiwa ni pamoja na kupokelewa vizuri na mashabiki wa Taarabu nchini.

“Namshukuru mungu kazi hii imepokelewa vizuri na mashabiki wangu, kwani tasnia ya muziki sasa ina wasanii wengi sana hadi kazi yako ikikubalika ujue umefanya kazi nzuri na umeumiza sana kichwa,” alisema.

Alisema kwasasa yupo katika mchakato wa kuachia video ya kazi hiyo ambayo anaamini itafanya vizuri pia kutokana na mazingira ambayo ameyatumia kutengeneza kazi hiyo

No comments :

Post a Comment