Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, June 18, 2013

REDDS MISS KINONDONI TALENT 2013 KUFANYIKA ALHAMIS 21 JUNI UKUMBI WA SHEKINAH GARDEN JIJINI DAR




Warembo wa Redds Miss Kinondoni 2013 wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutambulishwa mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani), kwa sasa warembo hao wameshaingia katika hoteli ya JB Belmont jijini Dar es Salaam kujinoa kwa ajili ya Redd's Miss Kinondoni Talent 2013 zinazofanyikia ukumbi wa Shekinah Garden Mbezi Beach na Fainali zinafanyika Juni 21 ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip.
---
Na Cathbert Angelo, Kajunason Blog.
SHINDANO la Redd’S Miss Kinondoni Talent 2013 linatarajiwa kufanyika alhamisi ya Juni 25 katika ukumbi wa Shekinah Garden, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam ambalo litashirikisha warembo wapatao kumi na mbili ambao watachuana kumpata mrembo mwenye kipaji.
Akizungumza mratibu wa shindano hilo, Dennis Ssebo alisema maandalizi ya kuelekea shindano hilo yanaendelea vizuri na kueleza mshindi atakabidhiwa zawadi zake kwenye fainali ya shindano hilo ambalo litafanyika Juni 21 mwaka huu katika uwanja wa hoteli ya Golden Tulip.
“Ninachoweza kusema shindano la mwaka huu litakuwa la aina yake kutokana na kusheheni warembo bomba wenye mvuto na hivyo kuonyesha kutakuwa na mchuano mkali miongoni mwao “Alisema Ssebo.
Warembo warembo wanaotarajiwa kumenyana ni kutoka katika vitongoji vya Sinza, Ubungo na Dar Indian Ocean ambao kwa pamoja wanaunda Redd's Miss Kinondoni 2013.
Alisema kwamba shindano la mwaka huu litaandika historia mpya ya urembo kwa wilaya ya Kinondoni maana wamejipanga na kupata sapoti ya kutosha, hivyo mashabiki wa mashindano ya urembo wakae mkao wa kupata raha.
Mashindano ya Redd's Miss Kinondoni yamedhaminiwa na Redd's Original, Chilly Willy Energy Drink, Oriflame Natural Beauty Products, Times Fm, JB Belmonte Hotel, Michuzi Media Group, Michuzijr Blog, Mtaa Kwa Mtaa Blog, Fullshangwe Blog, HandeniKwetu Blog, Mrokim Blog, TheHabari.com, JestinaGeorge Blog, SufianMafoto Blog, Global Publisher, Mdimuz Blog, Lukaza Blog, MO Blog na Kajunason Blog.

No comments :

Post a Comment