Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, July 3, 2010

TBL yaipiga jeki timu ya taswa fc ya arusha

Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari za michezo ambaye pia ni Mratibu wa tamasha la waandishi wa habari za michezo,Jamila Omari akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha hilo la michezo linalotarajia kufanyika Agost 1 mwaka huu.katikati ni Meneja matukio wakanda ya kaskazini wa TBL,George Mombeki na kushoto ni Katibu wa chamacha waandishi wa habari za michezo,Mussa Juma
Nahodha wa timu ya Taswa FC ya mkoa wa Arusha Moses Kilinga akikabithiwa jezi na mpira na mratibu wa tamasha hilo Jamila Omary kwa ajili ya maandalizi ya timu yake.
Meneja matukio wakanda ya kaskazini wa TBL,George Mombeki akimkabithi Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari za michezo ambaye pia ni Mratibuwa tamasha la waandishi wa habari za michezo,Jamila Omari mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni mbili iliyotolewa na kampuniya bia ya TBl kwa ajili ya mashindano hayo.


Na Woinde Shizza,Arusha

kampuni ya bia ya TBL imetoa cheki ya shilingi milioni mbili kwa ajili ya kudhamini Tamasha michezo la waandishi wa habari linalotarajia kufanyika Agosti moja mwaka huu katika kiwanja cha kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari za michezo mkoani hapa ambaye pia ni mratibu wa mashindano haya Jamila Omary wakati akiongea na waandishi wa habari alisema kuwa tamasha hili linatarajia kufanyika Agosti moja mwaka huu na litashirikisha jumla ya timu kumi na mbili zilizopo mkoani hapa.

Alisema kuwa tamasha hili hufanyika kila mara na linashirisha timu za waandishi wa habari kutoka katika mikoa mbalimbali ikiwemo timu ya waandishi wa habarikutoka mkoani Dar es salaam,Arusha pamoja na mkoa wa Manyara.

Alitaja nia ya tamasha hili ni kuwakutanisha pamoja waandishiwa habari kutoka katika mikoa mbalimbali pamoja na kuwapa burudani ikiwemo yamichezo mbalimbali na kubadilishana ujuzi na mawazo kwa ujumla.

Jamila alitaja timu ambazo zimejitokeza kushiriki katika mashindano haya kuwa ni Taswa FC ya Arusha,Taswa ya Dar ,timu ya chuo cha waandishi wabahari cha Arusha (AJTC),chuo cha waandishi wa habari east afrika ,radio five,triple A radio,Ormame radio ,timu ya CRDB,timu ya NMB,timu ya NSSF,timu ya Pepsi pamoja na timu kutoka kampuni ya bia ya TBL.

Akikabithi cheki hiyo meneja matukio wa kanda ya kaskazini kutoka TBL George Mombeki alisema kuwa kampuniu yao imehamua kuthamini tamasha hili kwani waandishi wa habariwamekuwa wakiwapa ushirikiano mkubwa sana.

"tumeamua kuwaunga mkono waandishi wa habari kwakuwa wamekuwa wakitupa ushirikiano mkubwa sisi pamoja na wananchi kwa ujumla na tunahaidi kuthamini mashindano haya mpaka mwisho hatutaishia hapa"alisema Mombeki.

No comments :

Post a Comment