Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, July 18, 2010

Thierry Henry astaafu soka ya kimataifa

Mchezaji mashuhuri wa timu ya Taifa ya Ufaransa na Barcelona Thierry Henry ametangaza kustaafu soka ya kimataifa na timu ya Taifa.

Henry mwenye umri wa miaka 32 ametangaza uamuzi huo wakati wa mahojiano na shirika la habari AP kabla ya kufikia uamuzi wa kujiunga na klabu ya mpira wa miguu ya New York Red Bulls.

Amesema kuwa anajiunga na klabu ya Red Bulls nchini Marekani, siyo kwa kutaka kumuiga David Beckham kwa kusafiri mara kwa mara baina ya Ulaya na Marekani.

Amesema huu ndiyo mwisho kwake kushiriki timu ya Taifa.

Thierry Henry

Thierry Henry

Tangu ajiunge na timu ya Taifa, Henry amefunga magoli 51 mara 123 alizoshiriki michuano ya kimataifa kwa niaba ya Ufaransa kuanzia mwaka 1997.

Alitia fora wakati akichezea klabu ya Arsenal ambako alikuwa nahodha na anatazamiwa kushiriki pambano la Red Bulls dhidi ya mahasimu wakuu wa klabu yake ya zamani, Tottenham hotspurs hapo tarehe 22 Julai.

Alipohama kutoka Arsenal mnamo mwaka 2007, Henry alijiunga na Barcelona ya Uhispania na alikuwa na mwaka mmoja uliosalia kwenye mkataba wake aliporuhusiwa na Barcelona kuweza kuihama.

No comments :

Post a Comment