Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, July 3, 2010

ziff kuanza rasmi julai 10,2010


Mkurugenzi wa Tamasha la ZIFF,Dr. Martin Mhando akifafanua jambo kwa wadau waliofika katika mkutano wa ufunguzi rasmi wa tamasha hilo uliofanyika leo katika ukumbi wa Alliance Francaise jijini Dar.
Mratibu wa Maswala ya Muziki wa ZIFF,Edward Lusala (kushoto) akitaja list ya wasanii watakao panda jukwaani katika tamasha hilo linalotazamiwa kuanza rasmi Julai 10 mpaka Julai 18 huko kisiwani Zanzibar.wengine toka kulia ni Dean Nyalusi (Meneja wa ZIFF),Dr. Martin Mhando (Mkurugenzi wa ZIFF) na Ibrahim Mitawi (Msaidizi wa mambo ya Kiufundi ZIFF).
Baadhi ya wadau walifika leo katika ufunguzi rasmi wa tamasha la ZIFF katika ukumbi wa Alliance Francaise jijini Dar wakifuatilia kwa makini maelezo ya Dr. Mhando (hayupo pichani)..


ZANZIBAR INTERNATIONAL FILM FESTIVAL


Zanzibar International Film Festival (July 10th-18th) ni tamasha kubwa kuliko yote ya utamaduni ya aina yake kwenye ukanda wa Afrika mashariki. Ikiwa imetimiza miaka 13 na kuudhuriwa kila mwaka na zaidi ya wageni 200,000 na kushirikisha nchi 43, ZIFF ni taasisi ya wazanzibari yenye kulenga zaidi filamu za kiafrika huku ikisherehekea na kuthamini utajiri wa tamaduni zilizopo ndani ya ukanda huu na zaidi

Tofauti na tamasha lingine lolote, hili ni tajiriba ya aina yake ya tamaduni za kiafrika. Hakuna zuria jekundu, Umaridadi na waandishi wa habari za udaku.

ZIFF ni tamasha linalokuja mara mmoja tu kwa mwaka, ni nafasi ya pekee kwa Wazanzibari kujumuika pamoja na kutazama filamu kwenye viwambo vikubwa. Kwa mwaka huu filamu zote zitaonyeshwa bure kwa wakazi wote wa Zanzibar!


ZIFF’s theme this year’s is Hopes in Harmony.
Mwishoni mwa mwaka huu Zanzibar itafanya uchaguzi mkuu wa serikali. Kuna historia ya machafuko kipindi cha uchaguzi kwa kutazama uchaguzi uliopita mwaka 2005 kati ya wanaounga mkono upinzania na polisi. Mbiu ya tamasha kwa mwaka huu ina angaz matakwa ya watu wa kisiwa hiki ya amani na muafaka.

Filamu ya ufunguzi, ni filamu yenye tunzo inayo muhusu mwanamziki maarufu Youssou N’Dour, I Bring What I love (Naleta nachokipenda), inayozungumzia ]addresses the themes of religious tolerance, harmony and peace.

“I Bring What I Love” imedhaminiwa na SIGNIS.


Key Facts & Figures in 2009
• Waudhuriaji Mji Mkongwe: 45,000
• Waudhuriaji Dar es salaam: 200,000
• Wageni toka nje: 12,000
• Nchi zilizo shiriki: 43
• Filamu zitakazoonyeshwa mwaka huu: 100


Vitu Vya Kutazamia Mwaka Huu…
Fainali ya Kombe la dunia! Kwa kuzindua tamasha 2010 tutaonyesha mechi ya fainali ya kombe la dunia ndani ya Ngome Kongwe.

Filamu ya ufunguzi
Youssou N’Dour. I Bring What I Love Ni filamu yenye tunzo nyingi. Ya kuhamasisha, inayotupeleka kwenye safari ya kimziki, yenye ushuhuda wa nguvu ya sauti ya mtu mmoja kuhamasisha mamilioni. Muongozaji wa Filamu: Elizabeth Chai Vasarhelyi. Imedhaminiwa na SIGNIS.

Nipe Jibu: Kuonyeshwa kwa mara ya kwanza . Filamu ya kwanza ya kuchanganya Muziki na kuigiza Muongozaji Nadine Louise Fasera. Nipe Jibu ni filamu nzuri ya Kiswahili yenye kuchanganya muziki iliyotengenezwa kwa mtazamo wa kisasa na kitamaduni kwa simulizi iliyochangamka juu ya binti yatima anayeishi kwenye maisha ya ndoto.

My Policy: Kuonyeshwa kwa mara ya kwanza. Kijana mdogo mfanya biashara anapigwa risasi kwenye siku yake ya kuzaliwa akiwa anarejea nyumbani kwake akitokea kwenye tafrija yake kusherehekea siku hii muhimu akiwa na mchumba wake, Victoria. Wiki chache baadae, Yule aliyempiga risasi amjia na kumchoma kisu hadi kufa. Kwa kupagawa na pigo hili, Victoria aamua kuhama Montreal na kuanza maisha mapya, Lakini muuaji amjia nay eye pia.... Muongozaji: Phad Mutumba

Motherland: African premiere - Kuonyeshwa kwa mara ya kwanza Africa

Ana’s Playground: African premiere

Lamu’s Maulid: world premiere

Inside Life: world premiere
Pumzi: East Africa’s first ever science fiction film
A sneak preview of Twiga Stars

Muziki
ZIFF 2010 Itakua ikisakata kwenye burudani ya muziki na… Dully Sykes – AKA Mr Misifa ama Mr Chicks, Msanii anayetambulika sana kwa miondoko ya dancehall Tanzania. AY, Msanii anayengara ndani ya Africa Mashariki akiwakilisha vyema Tanznia na balozi wa burudani Tanzania, Kidumu , Ndiye mwanamuziki maarufu Africa Mashariki toka Burundi anayeshikilia Tunzo nyingi ikiwemo tunzo ya Muziki bora wa Afrika Mashariki kwa Tunzo za Tanzania Music Awards, Body Mind Soul Bendi ya watu 6 kutoka Kaskazini mwa Malawi wanaopiga mziki wa kiafrika wenye vionjo vya Jazz, Windhund featuring Sekembuke & Siga bendi kutoka Austria inayotumia vionjo vya kizungu na kiafrika, ushairi na sanaa ya simulizi ili kuleto vionjo vipya na vya aina yake kwenye ulimwengu wa muziki.

Filamu za Watoto!
Kwa kushirikiana na taasisi ya filamu ya Kidanish, Maonyesho ya filamu za Watoto zitaonyeshwa makundi makubwa ya Watoto, zikiwa zimetafsiriwa kwa Kiswahili kwajili ya Watoto na vijana wa Mji mkongwe.

Art exhibtions
"Hopes in Harmony" (Matumaini yenye Kuafikiana) – Onyesho la picha yanayoletwa na mpiga picha toka Italy, Carlo Deste
"Colour Bash" – Uchoraji wa vitenge kutoka pande mbalimbali za Afrika, na Mahelia de Randamie
Artwork kutoka wakina mama wa Iranian, Hii inaletwa na Ubalozi wa Iranian embassy
kwa kushirikiana na Soko Filam, ambapo watengeneza filamu na wachongaji toka Zanzibar wanakuja kuonyesha na kuuza bidhaa zao..

Tasnia
ZIFF ni tukio muimu kwenye jumuiya ya Cinema duniani. Festival Forum na Festival of Festival program inatoa nafasi kwa wasambazaji, mapromota, waongozaji wa filamu na waandaji kukutana ili kukomaza mizizi kwenye tasnia ya filamu kwenye nchi zinazoendelea. Mwaka huu wawakilishi toka Trinidad na Tobago, Uganda, Holland, Iran, Mexico and Italy watashiriki ZIFF kujadili nafasi ya matamasha ya filamu kwenye nchi zinazoendelea.

Warsha
ZIFF itaendesha warsha tatu wakitoa upendeleo kwa ushiriki wa waandaji filamu toka ukanda huu wa Afrika mashariki kwa waandaji wenye kuonyesha hari na vipaji vyenye mlengo wa kuibuka kwenye tasnia hii.

WARSHA ZA NAMNA YA KUOMBA MISAADA YA KIFEDHA KUANDAA FILAMU NA WARSHA – warsha itaongozwa na wakufunzi toka Sweden and Uganda

UANDAAJI WA MAKALA: CONNIE FIELD – Warsha hii ya siku nzima italeta mtazamo mzima wa namna ya kuandaa makala chini ya usimamizi wa mshikiliaji wa tunzo ya uandaaji wa makala(producer / director), Connie Field.

CINEPHILMS:UTENGENEZAJI WA FILAMU KUTUMIA SIMU YA MKONONI – Hii warsha ya aina yake itaongozwa na Jonathan Dockney wa chuo kikuu cha Natal South Africa. Utengenezaji wa filamu kwa kutumia simu za mkononi ni teknolojia inayo ibuka kwa kasi sana. Njo ujifunze jinsi ya kutengeneza filamu kwa simu!

Tafadhali bonyeza hapO kwa maelezo zaidi:
www.ziff.or.tz
ama
www.ziff.or.tz/press

Asmah Makua
(Swahili Press)
asmahmakau@yahoo.co.in
Tel no: 0713711413
Laura Martin-Robinson
(English language Press)
press@ziff.or.tz
Tel: +255 782689845

No comments :

Post a Comment