Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, January 14, 2014

Hemba aiangukia serikali, wadau wa dansi




Hemba (kushoto) akiwa na Hassani Bitchuka
MWANAMUZIKI wa bendi kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde', Abdallah Hemba, ameiomba serikali na wadau wa muziki kwa ujumla kusaidia kuupiga tafu muziki wa dansi kwa madai ndiyo kutambulisho halisi cha muziki wa Tanzania
Aidha amewataka wanamuziki wenzake kupendana na kusaidiana katika shida na raha kama wafanyavyo wasanii wa fani nyingine ili kujenga umoja na mshikamano.
Akizungumza na MICHARAZO katika mahojiano maalum, mtunzi na muimbaji huyo, alisema dansi limekuwa likichechemea kutokana na kutopata sapoti ya kutosha kama fani nyingine kitu ambacho alisema mwaka 2014 uwe wa mabadiliko na muziki huo kupewa kipaumbele.
Hemba, aliyewahi kutamba na Mchinga Sound na Super Sikinde Sound, alisema wapo wadau wa muziki huo wamekuwa wakiwaangusha kwa kutoupa kipaumbele katika nafasi zao hasa watangazaji na kuufanya muziki wa dansi hudorore.
Pia alisema ni lazima wanamuziki wa miondoko hiyo wapendane na kusaidiana kusaidia kujenga udugu na mshikamano utakaofanya wasonge mbele katika medani ya muziki nchini.

No comments :

Post a Comment