Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, January 23, 2014

MATENGENEZO DARAJA LA MKUNDI YAANZA, WAZIRI MAGUFULI AELEKEZA KAZI KUFANYIKA USIKU NA MCHANA, MAGARI KUANZA KUPITA IJUMAA



Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa watendaji wa Tanroads.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa anafuatilia kazi katika moja ya mitambo ya barabara.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika ukaguzi wa eneo lililobomolowa na mafuriko ya mvua katika daraja la Mkundi, Dumila mkoani Morogoro.
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza mmoja wa madereva wa Lori zinazofanya kazi katika eneo hilo.
Mtambo ukiwa kazini
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuelekeza dereva wa lori kumwaga mawe sehemu husika.
Muonekano wa Daraja hilo.


Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo ametembelea eneo la Dumila ambako mvua kubwa zinazoendelea kunyesha zimesababisha mafuriko ambayo yameharibu sehemu ya barabara kwenye daraja la Mto Mkundi mkoani Morogoro.

Akiwa katika eneo hilo Waziri Magufuli baada ya kujionea hali halisi amemwagiza Kaimu Mtendaji Mkuu wa Tanroads Mhandisi Crispianus Ako pamoja na Watendaji wengine waandamizi kutoka Tanroads na Wizara ya Ujenzi kuwepo hapo muda wote wakati kazi za kurejesha mawasiliano zikiendelea ili kuhakikisha kuwa matengenezo hayo yanakamilika kesho siku ya Ijumaa tayari kwa magari kuanza kupita.

Katika hatua nyingine Mhe. Magufuli ametahadharisha kuwa magari yanayoruhusiwa kuzungukia barabara mbadala inayoanzia Dumila kupita Kilosa hadi Morogoro ni mabasi ya abiria na magari mengine yasiyozidi uzito wa tani 10. “Barabara hii mbadala ya kupitia Kilosa, Melela hadi Morogoro ni ya mkoa na iko katika kiwango cha changarawe ikiwa na madaraja yenye uwezo wa kubeba chini ya tani 10 tu, hivyo magari mengine yote yenye uzito zaidi ya hapo yatabidi kusubiri wakati tukiendelea na jitihada za kuifungua barabara hii mapema iwezekanavyo” amefafanua Mhe. Magufuli.

Daraja la Mkundi liko kiasi cha kilometa 65 kutokea Morogoro mjini kuelekea Dodoma na mikoa mingine ya kati hadi magharibi mwa nchi yetu ikiungana na nchi jirani za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya watu wa Kongo.

No comments :

Post a Comment