Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, January 14, 2014

NEWS ALERT.AJALI MBAYA YA BASI LA SHABIBY NA PRINCES MUNAA



Abiria 28 wakiwemo watoto wanne wamejeruhiwa baada ya basi walilokuwa wamesafiria la Kampuni ya Shabiby kugongana na Lori tupu la mafuta na kupinduka katika kijiji cha Kisaki umbali wa kilometa 10 kwenye Barabara Kuu ya kutoka Mjini Singida kwenda Dodoma.
Taarifa zilizopatikana kwenye eneo la tukio zimeelezwa kuwa Basi hilo lenye namba T930BUW aina ya Yutong  lililokuwa likiendeshwa na Dereva wake ambaye
amekimbia mara baada ya ajali hiyo linakadiriwa kuwa na abiria wapatao 48 lilipata ajali hiyo jana saa 6:50 mchana wakati lilipojaribu kulipita lori hilo upande wa kulia .
Taarifa hizo ambazo pia zimethibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Singida zinasema kuwa kitendo hicho kilisababisha kuligonga Lori hilo RAA 496N aina ya MECEDES BENZ lililokuwa likitokea Mjini Kigali nchini Rwanda kwenda Dar es Salaam likiwa na dereva wake Barimana Benjamini (37) na kuanguka upande wa kulia wa Barabara na kujeruhi abiria wake .Habari picha kwa hisani ya superfeoblog.com

No comments :

Post a Comment