Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, November 15, 2014

REDBULL WAMLETA BINGWA WA KUPIGA MISELE NA PIKIPIKI KUTOKA AFRIKA KUSINI


MWANAMICHEZO ambaye anacheza kwa kutumia chombo cha moto Pikipiki  Bryan Capper yuko nchini kwa mwaliko maalum akitoka nchini kwao Afrika kusini ametoa wito kwa watanzania kucheza mchezo huo ambao mbali ya kufurahisha pia unatumia akili na kukufanya uwe mkakamavu wakati wote.
Akizungumza leo asubuhi  katika viwanja vya Coco Beach  Jijini Dar es Salaam ambako ndiko alikoanza kuonesha onyesho lake la kwanza  na kuonesha umahiri wake katika uendeshaji wa pikipiki  yupo nchini kwa kudhaminiwa na Kampuni ya Red Bull, atakuwa nchini kwa ziara ya  siku tatu.
Kesho  Jumapili atakuwa katika viwanja vya Mlimani City na  Jumatatu atahitimisha ziara yake katika eneo la Ubungo Tanesco.
Capper amesema kwamba amefurahia kuweza kufika nchini Tanzania  pia tayari ameshafanya maonyesho yake katika nchi za Kenya na Uganda.
Wakati huohuo Rais wa Tanzania Motorcross Acrobatic Club , Blagina Mwihava alisema kwamba wamemleta  mwanamuchezo huyo ambaye wana imani kubwa ataleta msisimko mkubwa kwa vijana wa kitanzania kuweza kupata hamasa ya kucheza mchezo huo wenye mvuto.    
 “Hii itakuwa ni shoo kwa watanzania  ili waweze kuvutika kucheza mcheo huu wa aina yake .

Ziara ya mchezaji huyo imeratibiwa na Kampuni ya Mohans  inayosambaza kinywaji cha Redbull nchini maonesho hayo yote  ni ya wazi.

No comments :

Post a Comment