Familia ya Mwanamuziki Nguza Viking imemuomba Raisi Jakaya Kikwete kuingilia kati suala la kuendelea kukaa gerezani kwa mwanamuziki huyo na mwanaye JohnSon Nguza maarufu Papii Kocha.
Ombi hilo limetolewa leo na shangazi wa nguza viking, bibi Mwisha Matuka Bizoo, baada ya mahaka ya Rufaa kuwaachia huru, watoto wao, Francis Nguza na Nguza Mbangu na kumrejesha Gerezani mwanamuziki huyo na mwanawe Papii Kocha.
Nguza Viking, na watoto wake watatu walihukumiwa kifungo cha maisha Jela mwaka 2004 na mahaka ya hakimu mkazi kisutu Jijini Dar es Salaam baad ya kupatikana na hatia ya kuwadhalilisha kijinsia waoto wa kike eneo la sinza jijini.
Hata hivyo, baada ya hukumu iyo kupitiwa upya na majaji wa tatu, Bwana Salum masati, Bwana Mbaruk Mbaruk, wakiongozwa na Bwana Nathalia Kimaro, makama hiyo imebaini kuwa watoto wawili wa Nguza Viking, Fransis Nguza na Nguza Mbangu walifungwa kimakosa.
Akisoma huku hiyo, Jaji Neema Chusi, amesema wakati makosa hayo yakifanyika jijini Dar es Salaam, Nguza Mbangu, alikuwa kwenye ziara za kimuziki, na Fransis Nguza, alikuwa Shuleni.
No comments :
Post a Comment