Akiongea na kipindi cha michezo na burudani cha Radio Times FM Afisa habari wa Simba Cliford Ndimbo amesema kuwa mchezo huo ni maandalizi ya michuano kombe la Shirikisho barani Afrika CAF itakayoanza marchi mwaka huu.
Ndimbo ametaja viingilio katika mchezo huo kuwa VIP 10,000, na kuna viti vya Tshs 5000 na 3000.
Aidha amewataka mashabiki wa kandanda kujitokeza kwa wingi kuwaungana kama ambavyo wamekuwa wakiwaunga mkono katika michezo ya ligi kuu Tanzania Bara.
Siku ya JUmapili Machampion hao wa Zambia timu ya Zesco itacheza na klabu ya Azam FC ambayo inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.
No comments :
Post a Comment