Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, April 15, 2012

Mama yake Kanumba atoa wosia kwa SHIWATA






Na Peter Mwenda

MAMA Mzazi wa aliyekuwa msanii wa filamu nchini marehemu Steven Kanumba amewataka wasanii wanachama wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) kuendeleza ushirikiano alioacha mwanae.

Akizungumza katika ibada ya kumuombea mwanae iliyoandaliwa na M (SHIWATA) leo Dar es Salaam, Mama Kanumba alisema amefarijika kuona wasanii wanaendelea kumuombea mwanae kila kona ya nchi.

"Nawashukuru SHIWATA kwa moyo wa ipendo na ushirikiano mlionesha kwa familia yangu, naomba muendeleze ushirikiano mliokuwa nao wakati mwanangu akiwa nanyi, endeleeni kushirikiana" alisema Mama Kanumba.

Katika ibada hiyo iliyoongozwa na mchungaji wa Kanisa la Elim Pentekoste Ilala Bungoni, Mchungaji Livingstone Mwaitela alisema wasanii na familia ya Kanumba wasisononeke kwa sababu Mungu alimpenda mtoto wao huyo zaidi.

Alisema wasanii waendelee kumkumbuka mwenzao kwa kubadili mambo yasiyompendeza Mungu badala yake wajiandae kwa kufanya mambo ambayo yanampendezesha na kujiweka tayari siku akiwaita wawe tayari.

Mwenyekiti wa SHIWATA,Caasim Taalib alisema Kanumba alikuwa mwanachama wao namba 648 akiwa mmoja wa waliojitokeza kutafuta eneo kwa ajili ya kujenga nyumba za wasanii kutoka Bagamoyo, Kisarawe na hatimaye kufanikiwa kupata eneo Mkuranga.

Marehemu Kanumba alifariki Aprili 5, wakati akikimbizwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) baada ya kuanguka nyumbani kwake Sinza kufuatia ugomvi wa mapenzi na msanii mwenzake Elizabeth Michael (Lulu).

No comments :

Post a Comment