![]() |
FFU wa Ngoma Africa Band wameachia Jipya "Uhuru wa Habari" Unasikika at www.ngoma-africa.com Kwa kawaida wanahabari na vyombo vyao ndio wanarusha hewani habari za matukio mbali mbali pamoja wasanii na burudani zao kwa jamii, Lakini bendi maarufu Ngoma Africa aka FFU imewageuzia kibao !! Kuliweka hewani song jipya "Uhuru wa habari" wimbo huo mpya utunzi wake kamanda Ras Makunja akiimba kwa kushirikiana na kijana Christian Bakotessa aka Chris-B,ambaye pia ni mpiga gitaa la solo(mtutu) wa kikosi kazi iko. Bendi hiyo maarufu Ngoma Africa yenye makao yake kule ujerumani, miezi michache tu iliachia hewani CD ya "Miaka 50 ya Uhuru" na sasa wanarusha hewani "Uhuru wa habari" , Taarifa za kuhaminika zinaeleza kuwa Remix ya wimbo huo pia itakua hewani siku za usoni,katika Remix hiyo kutakua na majina mengi ya wa dau wa habari ambao wanachangia kuijulisha jamii habari mbali mbali. Sikiliza na pata burudani ya bure katika ffu camp at www.ngoma-africa.com |
WAKAZI WA DAR ES SALAAM WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA UPASUAJI WA MABUSHA BURE
-
*Wizara ya Afya imeanza kambi maalum ya siku 30 ya upasuaji na uchunguzi
wa magonjwa ya mabusha na matende kwa wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam.*
*Kamb...
1 day ago

No comments :
Post a Comment