Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, April 14, 2012

ULIMWENGU ATUA NGORONGORO HEROES



Ulimwengu

Mshambuliaji Thomas Ulimwengu ambaye ndiye mchezaji pekee kutoka nje aliyeitwa na Kocha Kim Poulsen kwenye U20 (Ngorongoro Heroes) anatarajia kujiunga na kikosi hicho ambacho kiko kambini kesho (Aprili 14 mwaka huu).
Ulimwengu ambaye anachezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) atawasili saa 1.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways akitokea jijini Lubumbashi.
Ngorongoro Heroes ambayo iliingia kambini Aprili 20 mwaka huu inajiandaa kwa mechi ya mashindano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 dhidi ya Sudan. Mechi hiyo itachezwa Aprili 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Kwa mujibu wa Kocha Poulsen, kikosi chake kesho (Aprili 14 mwaka huu) kitakuwa na awamu (sessions) mbili za mazoezi kwenye Uwanja wa Karume. Awali ya kwanza itakuwa asubuhi nay a pili itafanyika jioni.
Wachezaji wengine walioko kwenye kikosi hicho cha Ngorongoro Heroes ni Saleh Malande, Aishi Manula, Hassan Kessy, Said Ruhava, Carlos Kilenge, Dizzana Issa, Amani Kyata, Issa Rashid, Emily Mgeta na Khamis Mroki.
Wengine ni Ramadhan Singano, Frank Sekule, Frank Domayo, Omega Seme, Abdallah Hussein, Ibrahim Rajab, Hassan Dilunga, Alhaje Zege, Jerome Lambele, Atupele Green na Simon Msuvan.
Mechi ya marudiano dhidi ya Sudan itachezwa jijini Khartoum kati ya Mei 4, 5 na 6 mwaka huu.
Fainali za Afrika kwa vijana zitafanyika Machi mwakani nchini Algeria. Timu nne za juu kwenye fainali hizo zitacheza Fainali za Dunia zitakazofanyika nchini Uturuki kuanzia Juni hadi Julai mwakani.

No comments :

Post a Comment