SHIRIKISHO
 la Ngumi la Kimataifa (IBF) pamoja na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa 
Tanzania (TPBC) vyatuma salamu za rambirambi na kumlilia bingwa wa IBF 
wa mabara na bingwa wa dunia wa WBU Magoma Shaban.
Magoma
 aliyefariki jana katika hospitali ya Bombo jijini Tanga atakumbukwa kwa
 umahiri wake katika mchezo huo wa ngumi za kulipwa.
Safari
 ya Magoma Shaban kwenye ngumi za kulipwa ilianzia katika uwanja wa 
Mkwakwani jijini Tanga mwaka 1998 wakati Onesmo Ngowi akiwa ndio kwanza 
ameteuliwa na Rais wa zamani wa IBF Robert Lee Sr, kutoka nchini 
Marekani kuanzisha shirikisho hilo la IBF katika bara la Afrika.
Katika
 pambano hilo lililofanyika uwanja huo wa Mkwakwani, Magoma Shaban, 
alipigana na Joseph Waweru kutoka Kenya na kumshinda kwa KO na 
kutangazwa kuwa bingwa wa IBF katika bara la Afrika uzito wa Flyweight.
Mwaka
 2000 Magoma chini ya kamouni ya Capital Promoters Limited chuini ya 
mwandishi wa bahari mahiri bwana Gabriel Nderumaki alipigana na bondia 
Totim Lukunim toka Thailand katika ukumbi wa PTA kugombea mkanda wa IBF 
wa mabara katika uzito wa Flyweight na kumshinda  kwa KO katika raundi 
ya 4. Huo ndio ukawa mwanzo wa magoma Shaban kwenye kwenye matawi ya juu
 katika ngumi.
Magoma Shaban alipigania ubingwa wa dunia wa WBU nchini Italy na kumshinda bondia Ferid Ben Jeddou kwa TKO katika raundi ya 6.
Magoma alikuwa ni bondia aliyeing'arisha Tanzania na bara zima la Afrika katika medani ya ngumi za kulipwa duniani.
Kwa
 mantiki hiyo leo IBF imetangaza rasmi kuuita mkanda wa uzito wa Fly 
aliokuwa anachezea Magoma kuwa "Mkanda wa Magoma Shaban" katika 
mapambano yote yatakayokuwa yanachezezwa katika uzito huu yatajulikana 
kama "Ubingwa wa IBF Africa wa Magoma Shaban".
Tunafanya
 hivi ili kuwaenzi mabondia wanaoleta mchango mkubwa katika medani ya 
ngumi na hivyo majina yao kubakia katika kumbukumbu zetu milele.
Mola alitoa na Mola ametwa, jina lake lihidimiwe milele. Amin!
 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments :
Post a Comment