Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, May 25, 2012

HALI BADO TETE YANGA LICHA YA NCHUNGA KUJIUZULU




KIKAO cha Kamati ya Utendaji ya Yanga kujadili barua ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Wakili Lloyd Baharagu Nchunga kujiuzulu kimeshindwa kufanyika leo, kutokana na safu kutotimia.
Katibu Mkuu wa Yanga, Celestine Mwesigwa ameiambia BIN ZUBEIRY mchana huu kwamba, Mbaraka Igangula yupo Afrika Kusini wakati Khalifa Mgonja yupo Arusha,
Mwesigwa alisema kwa sababu hiyo, wanasubiri Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji wafike Dar es Salaam ndipo kikao kifanyike. Wakati huo huo, Wazee wa klabu hiyo walikutana na waandishi wa Habari leo mchana makao makuu ya klabu na kusema kwamba, hawamtambui Mjumbe yeyote wa Kamati ya Utendaji, kwani Nchunga ameondoka na watu wake wote.
Aidha, baadhi ya Wajumbe waliotangaza kujiuzulu wameanza kuzikana barua zao, wakidai walilazimika kuandika kutokana na vitisho walivyokuwa wakipewa.  BIN ZUBEIRY iliwasiliana na Mwanasheria wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alex Mgongolwa kutaka ufafanuzi zaidi juu ya sakata la klabu hiyo, lakini akasema yuko kwenye kikao.
Wakati BIN ZUBEIRY ikiwa imetega rada zake kwa Mgongolwa hadi hapo atakapomaliza kikao, taarifa zaidi zinasema kikao hicho kinahnusu syala hilo hilo la Yanga na atalitolea tamko leo.
Jana, Nchunga alitangaza kujiuzulu Uenyekiti wa Yanga, akisema timu anaikabidhi kwa Baraza la Wadhamini, ambalo kwa sasa linaundwa na wajumbe watatu, Mama Fatuma Karume, Deo Filikunjombe na Francis Kifukwe.

No comments :

Post a Comment