Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, May 23, 2012

MAHAKAMA YAMGOMEA KAJALA HAKIMU MPYA



Kajala Masanja kuli, akiwa amejifunika usoni na kushoto katika pozi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imetupilia mbali maombi ya msanii wa filamu nchini Kajala Masanja na mumewe Faraja Chambo ya kutaka kesi yao ihamishiwe kwa hakimu mwingine ili iweze kuendelea kusikilizwa. 
Kajala na mumewe waliwasilisha maombi hayo baada ya kupokea taarifa kuwa hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi yao Sundi Fimbo yupo likizo ya uzazi . 
Maombi yao yalitupiliwa mbali na Hakimu Frank Moshi ambaye alisema amepokea jalada la kesi hiyo kwa ajili ya kutoa ufafanuzi. 
“Nimewasiliana na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama Ilvin Mgeta , amesema kwa kawaida shauri halifanyiwi mabadiliko iwapo hakimu yupo likizo na kwamba huo utakuwa ni usumbufu,” alisema hakimu huyo. 
Baada ya uamuzi huo alipanga kesi hiyo iahirishwe hadi Juni 5, mwaka huu itakapotajwa mpaka hakimu atakapomaliza likizo yake. 
Kajala Masanja na mumewe Faraja Chambo wanakabiliwa na mashtaka matatu kula njama, kuhamisha umiliki wa nyumba na kutakatisha fedha haramu.

No comments :

Post a Comment