Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, May 23, 2012

KESI YA MINTANGA JUNI 11



Mintanga
MAHAKAMA Kuu yaTanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imepanga Juni 11 mwaka huu kuendelea kusikiliza ushahidi wa upande wa Jamhuri wa kesi inayomkabili aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (TBF), Shaabani Mintanga ya kusafirisha dawa za kulevya kilo 4.8. 
Kwa mujibu wa shajala ya Mahakama, kesi hiyo itaendelea kusikilizwa siku hiyo mbele ya Jaji Dk. Fauz Twaib, ambaye alikuwa akiisikiliza tangu mwanzo. 
Kesi hiyo iko katika hatua ya kusikilizwa mashahidi wa upande wa Jamhuri, ambapo mashahidi ambao wameshatoa ushahidi ni pamoja na Godfrey Mroso ambaye ni mfanyakazi wa Kampuni ya Anvelope Travel Agency, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) , Charles Ulaya na kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya ngumi, Nassoro Michael. 
Mintanga alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mwaka 2008, akikabiliwa na mashitaka ya kula njama na kusafirisha dawa za kulevya kilo 4.8.

No comments :

Post a Comment