Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, May 30, 2012

TUMBAKU HUUA WATU MILIONI 6 KWA MWAKA DUNIANI KOTE




NA MWANDISHI WETU
WAKATI Watanzania wakitarajia kudhimisha Siku ya Kutotumia Tumbaku Duniani kesho, imebainika kuwa tumbaku huua watu takribani milioni sita (6), kila mwaka.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Kumbana na Matumizi ya Tumbaku, Lutgard Kagaruki wakati alipokuwa akizungumza na wandishi wa habari katika Ukumbi wa Habari (Maelezo), jijini Dar es Salaam kuhusu Siku ya Kutotumia Tumbaku Duniani.
Alisema maradhi yabayosababishwa na tumbaku huathiri nchi zite duniani, na ndiyo maana jumuiya ya kimataifa ikaungana na Mkataba wa Kimataifa wa Shirika la Afya Duniani wa kudhibiti matumizi ya tumbaku.
Kagaruki alisema  Mkataba huo umebeba misingi muhimu ya udhibiti wa matumizi ya tumbaku, itakayoweza kuokoa maisha ya watu milioni 200 ifikapo mwaka 2050, kama itatekeleza ipasavyo.
Alisema muingiliano wa kampuni za tumbaku umekuwa tishio kubwa kuliko yote kwa mikakati ya kutekeleza mkataba wa kimataifa wa kudhibiti matumizi ya tumbaku.
Kagaruki alibainisha kuwa mkataba huo unavipengele muhimu kwenye Kanuni namba  5.3 ambacho kinaeleza bayana mgongano mkubwa wa maslahi uliopo kati ya kampuni za tumbaku na afya ya jamii.

No comments :

Post a Comment