Mchezaji wa zamani wa Klabu ya Manchester United ya Uingereza Quinton 
Fortune, akipiga mpira kuashiria uzinduzi rasmi wa michuano ya vijana 
wenye umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars. Uzinduzi huo 
ulifanyika jana, Mei 10, kwenye Hoteli ya Sea Clif, jijini Dar es 
Salaam.

 
Mchezaji wa zamani wa Manchester United ya Uingereza Quinton Fortunewa 
pili kulia, akionyesha waandishi wa habari (hawako pichani) baadhi ya 
vifaa vya michezo vitakavyotumika kwenye michuano ya soka ya kimataifa 
kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars jana 
kwenye Hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam. Kati ni Waziri wa 
Mawasiliano, Sayansi na Technologia Mh. Professa Makame Mbarawa, wa 
kwanza kulia ni Mkurugenzi Mashindano wa TFF Sandy Kawembe, Mkurugenzi 
Mtendaji wa Airtel Tanzania Sam Elangallor na Mkurugenzi Bidhaa Airtel 
Afrika Obina Justine.
KAMPUNI ya Airtel Tanzania imezindua awamu ya pili ya mpango wa kuibua 
na kusaka vipaji vya soka unaojulikana kama ‘Airtel Rising Stars’, zoezi
 lililoendeshwa na nyota wa zamani wa Manchester United, Quinton 
Fortune.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam, 
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sam Elangallor, alisema 
mafanikio ya mwaka jana yanaonyesha mpira wa miguu, una uwezo wa 
kuunganisha makabila mbalimbali na pia kuleta hamasa kwa jamii, kuanzia 
ngazi ya chini hadi taifa.
Alisema mwaka jana zaidi ya timu 11,000 Afrika, zilijiandikisha 
kushiriki kwenye michuano hiyo, kuanzia kwenye mtoano na kuchagua 
wachezaji ambao waliunda timu zilizoshiriki kwenye ngazi ya mkoa.
“Awamu hii ya pili, inafuatia ile ya kwanza ya mwaka jana kuwa na 
mafanikio makubwa. Lengo la mpango huu ni kuvipa vipaji vinavyochipukia 
chini ya umri wa miaka 17, nafasi ya kuonyesha vipaji vyao kwa makocha 
waliobobea na pia kupata nafasi ya kuendeleza vipaji vyao,” alisema.
Alisema kama ilivyokuwa kwa mwaka jana, mpango huu utaanzia ngazi ya 
mkoa, taifa na kufuatiwa na kliniki ya soka ya kimataifa chini ya 
wakufunzi kutoka klabu ya Manchester United ya Uingereza. 
Aliongeza kuwa mwaka huu kutakuwa na mashindano ya siku nne ya timu 
bingwa kutoka kila nchi itakayoshiriki michuano hiyo, kushindania taji 
jipya la Airtel Rising Stars African Champion.
“Tumeamua kuongeza mshindano ya nchi na nchi mwaka huu, kwa nia ya 
kuweza kuwafanya vijana kushirikiana na kuwaleta karibu kwa kupitia njia
 ya pamoja, ambayo ni mchezo wa kandanda. Tunaamini ya kwamba michuano 
hii italeta hamasa na umoja kwa wachezaji,” alisema.
Kwa mwaka huu, michuano hii imezinduliwa na mchezaji wa zamani wa 
Manchester United, Quinton Fortune, ambaye alisajiliwa na Sir Alex 
Ferguson mwaka 1999, akitokea Atletico Madrid, wakati huo akiimarisha 
timu yake kushinda matajizaiti tembelea
http://mamapipiro.blogspot.com/
 
No comments :
Post a Comment