Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, March 18, 2014

Afande kuzichezea Yanga, Azam kesho viingilio vyatajwa



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgjwf5s6M54Nrjrxa-6oXNb65uDYGUeCjJHLWA9YMwLDx7YE5l5DQJ6RwXzML8g5xkHCjduPkBfBGqjuO4Z4rqf0MxXZ9zehgPXUH7Yb9nvHSqQwutGLO1ys6LxYl_hR7QNirGVaGfcBPI_/s1600/Yanga+Vs+Azam.JPG
Kesho shughuli itakuwa kama hii Taifa
REFA ambaye ni askari wa jeshi la Polisi Tanzania, Hashim Abdallah wa Dar es Salaam ndiye atakayechezesha mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Yanga na Azam itakayochezwa kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.
Hashim atasaidiwa na Anold Bugado wa Singida, Florentina Zablon wa Dodoma na Lulu Mushi wa Dar es Salaam, wakati Kamisaa atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya na mtathimini wa waamuzi ni Alfred Rwiza wa Mwanza.
Tiketi kwa ajili ya mechi hiyo zitaanza kuuzwa saa 2 asubuhi katika magari maalumu kwenye vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Ubungo Terminal, mgahawa wa Steers uliopo Mtaa wa Samora/Ohio, OilCom Ubungo, Buguruni Shell, Dar Live- Mbagala, kituo cha daladala Mwenge na Uwanja wa Taifa.
Baada ya Saa 6:00 mchana mauzo yote yatahamia Uwanja wa Taifa ambapo milango kwa ajili ya mechi itakuwa wazi kuanzia saa 7.30 mchana.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 30,000 kwa VIP A, sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani kiingilio ni sh. 7,000.

No comments :

Post a Comment