Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, March 24, 2014

SIMBA PWAAA, YAPIGWA 1-0 NA COASTAL UNION, AZAM YAZIDI KUPAA






TIMU kongwe ya soka nchini, Simba jana ilipigwa mweleka wa bao 1-0 na Coastal Union katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kipigo hicho kimepoteza matumaini ya Simba kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo baada ya kutokuwa na uwezo wa kushika nafasi mbili za kwanza.

Bao pekee na la ushindi la Coastal Union lilifungwa na mshambuliaji Hamad Juma dakika ya 44, kufuatia shambulizi kali lililofanywa kwenye lango la Simba.

Simba ilizinduka katika kipindi cha pili na kufanya mashambulizi kadhaa kwenye lango la Coastal Union, lakini juhudi za washambuliaji wake kusaka bao la kusawazisha hazikufanikiwa.

Kiungo Jonas Mkude ndiye aliyefanya majaribio mengi kwenye lango la Coastal Union kwa kupiga mashuti makali matano, lakini moja liligonga mwamba wa pembeni wa goli na mengine yalitoka nje.

Katika mechi zingine za ligi hiyo zilizochezwa juzi, Azam iliichapa JKT Oljoro bao 1-0 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Ashanti ilipigwa mweleka wa mabao 2-0 na JKT Ruvu mkoani Pwani.

No comments :

Post a Comment