Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, March 29, 2014

Ni Mwadui na Stand kupanda Ligi Kuu msimu ujao


Kocha wa Mwadui Shinyanga, Jamhuri Kihwelu 'Julio' akikaribia kuipandisha daraja timu hiyo


TIMU ya Mwadui Shinyanga imejiweka katika nafasi nzuri ya kupanda Ligi Kuu baada ya kuinyuka Toto Africans nyumbani kwao Mwanza kwa bao 1-0.
Mwadui inayofundishwa na Jamhuri Kihwelu 'Julio' kwa ushindi huo wa ugenini imefikisha jumla ya pointi 28 na imesaliwa na mechi moja, huku Toto Africans ikipoteza matumaini ya kurejea katika ligi hiyo.
Hii inatokana na Stand Utd pia ya Shinyanga iliyopo nafasi ya pili kuibutua JKT Kanembwa nyumbani kwao mjini Kigoma kwa mabao 3-2 na kufikisha jumla ya pointi 26 na kuendelea kuibana Mwadui ambao wamekuwa na upinzani mkubwa baina yao.
Toto iliyopo nafasi ya tatu imebakia na pointi 21 ambapo hata kama itashinda mechi yao ya mwisho haitaweza kuwafikisha popote na kuziacha timu pinzani za Shinyanga, Mwadui na Stand zikisubiri kujua hatma ya mmoja wao kupanda Ligi Kuu msimu wa 2014-2015 siku ya Aprili 5 mwaka huu.
Tayari timu mbili za Polisi Moro na Ndanda Fc zimeshafuzu ligi ya msimu ujao baada ya kuongoza kwenye makundi yao ya A na B.

No comments :

Post a Comment