Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, March 24, 2014

NSSF YATOA ELIMU KUHUSU HIFADHI YA JAMII KWA WANACHUO WA CBE


 Mkurugenzi wa Wanafunzi wanaochukua Mafunzo ya Shahada ya kwanza katika Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Dk. Esther Mbise akimkaribisha mgeni rasmi, Meneja Kiongozi Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii ( NSSF), Eunice Chiume (katikati),wakati wa Semina kwa wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), iliyofanyika katika chuoni hapo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Masoko chuoni hapo, Felix Chale. Jumla ya wanachuo 180 walihudhuria semina hiyo.
Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume akitoa mada wakati wa semina ya kuwawezesha wanafunzi wa vyuo vya Elimu ya Juu kuwa na uelewa kuhusu Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii  (NSSF), pindi watakapomaliza elimu yao.
Baadhi ya wanafunzi wakimsdikiliza kwa makini, Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume wakati akitoa mada katika semina hiyo.
 Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume akitoa mada kuhusu faida za kuwa mwanachama wa NSSF.
Tunasikiliza kwa makini.
 Baadhi ya maofisa wa NSSF wakigawa vibeberushi vyenye maelezo ya muhimu kuhusu NSSF.
Ofisa Uhusiano wa NSSF, Maife Kapinga akigawa vibeberushi kwa wanafunzi wa CBE wakati wa kongamano hilo.
 Tunajifunza hifadhi ya jamii.
 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha CBE wakisikiliza kwa makini kazi za mfuko wa hifadhi ya jamii na faida zake
 Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume akijibu maswali ya wanadunzi wa CBE kuhusiana na mfuko wa Taifa Hifadhi ya Jamii wa NSSF.
 Jonas Pera akiuliza swali.
 Mwanachuo wa CBE, Hadson Mwakilima akiuliza swali kuhusu mafao ya NSSF.
Mwanafunzi aliyejitambulisha kwa jina la Mohamed akiuliza swali.
Wanafunzi wakipewa zawadi za fulana za NSSF.
Ofisa Uhusiano wa NSSF, Maife Kapiga akigawa zawadi ya Kalenda za NSSF kwa wanafunzi wa CBE.
Ofisa Uhusiano wa NSSF, Said Mohamed akifafanua jambo wakati wa semina hiyo.

No comments :

Post a Comment