Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, March 24, 2014

AS Vita yaifyatua Kaizer Chiefs 3-0



http://www.michezoafrika.com/NewsImages/VIta-club-of-Congo.jpg
KLABU YA AS Vita ya DR Congo imeifumua Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini kwa mabao 3-0 katika mechi za 16 Bora Ligi ya Mabingwa Afrika, huku AC Leopards ya Kongo ikilazimishwa sare nyumbani na Al Hilal ya Sudan.
mabao yote ya Vita katika pambano hilo yalifungwa na Firmin Ndombe Mubele na kuiweka katika nafasi nzuri timu yake ya kufuzu robo fainali ya michuano hiyo iwapo itakomaa kwenye mechi ya marudiano wiki ijayo nchini Afrika Kusini.
Katika michuano ya Kombe la Shirikisho, Zesco ya Zambia ikiwa ugenini nchini Ghana imechezea kichapo cha mabao 2-0 toka kwa wenyeji wao Medeama, huku Ismailia ya Misri na Petro du Luanda ya Angola zikishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu.
Nayo timu ya Warri Woriors ya Nigeria imelazimishwa sare tasa na Bizertin ya Tunisia katika pambano jingine la mkondo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho.
Mechi nyingine za ratiba ya mkondo wa kwanza zinaendelea kuchezwa kwa sasa ukiwamo pambano la TP Mazembe dhidi ya wenyeji wao Sewe Sports ya Ivory Coast.

No comments :

Post a Comment