Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, August 11, 2014

Isike Samuel: Wasanii tuache wivu wa kijinga tusonge mbele



MUIGIZAJI na mtayarishaji wa filamu nchini, Isike Samwel amesema tabia za wivu, utengano na kutopendana miongoni mwa wasanii ndiko kunakofanya waendelee kulizwa na maharamia kwa kuwaibia kazi zao na kushindwa kusonga mbele.
Hivyo akawataka wasanii kubadilika na kupendana, kushirikiana na kusaidiana bila kujali uzoefu, umaarufu au uwezo wa kiuchumi walionao kwa vile wote wanasafiri katika 'jahazi' moja.
Akizungumza na MICHARAZO, Isike alisema gurudumu la fani ya sanaa hasa ya uigizaji imekuwa ikishindwa kusonga mbele kutokana na wasanii kutopendana na kuoneana kijicho pale mwenzao anapofanya vyema.
Isike alisema hivyo ni wajibu wasanii kubadilika kwani umoja, mshikamano na upendo itasaidia kuwafanya wawe kitu kimoja na kusaidia kupambana na watu wanaowanyonya na kuwaibia kazi zao wanazozitolea jasho kuziandaa.
"Bila umoja, upendo na ushirikiano ni vigumu fani yetu kusonga mbele, wasanii tumekuwa hatupendani wenyewe kwa wenyewe na watu wanaoneana wivu wa kijinga ambao unazorotesha maendeleo ya fani hiyo kwa ujumla," alisema.
Mkali huyo anayejiandaa kutoa filamu yake mpya iitwayo 'Naiogopa Kesho' kupitia kampuni binafsi ya Classic Vision alisema pia wasanii wazoefu wasiogope kuwapiga tafu chipukizi kwa hofu ya kufunikwa kwani hata wao waklisaidia na kupewa nafasi ndiyo maana wapo hapo walipo.

No comments :

Post a Comment