Maandalizi ya pambano la ngumi za kulipwa la kuwania ubigwa Afrika kwa Awadh Tamim dhidi ya bondia Ashrafu Suleiman pambano litakalopigwa katika ukumbi wa DDC mlimani jijini Dar es Salaam yamekamilika.
Akiongea na kipindi cha michezoi cha Radio Times FM mwandaaji wa pambano hilo Shomari Kimbau amesema kwamba pambano hilo linatakuwa upinzania wa hali ya juu kutokana na maandalizi kabambe yanayofanywa na mabondia hao.
Amesema sababu kubwa ya pambano hilo ni baada ya Awadhi Tamimu kutangaza kuacha wazi mikanda yake ya Ubingwa wa Tanzania na Afrika Mashariki na kuweka nia ya kuwania ubingwa wa Afrika lakini bondia Ashrafu Suleimani akataka wapambane ili kumuonesha kwamba kunamabondia wanauwezo.
Awadhi Tamimu alifikia maamuzi hayo ya kuachia mikanda hiyo wazi baada ya kukosa mpinzani, hivyo Ashrafu amesema anataka kumuonyesha kwamba anaweza.
Kimbau amesema Bingwa atakayepatikana katika pambano hilo ndiyo atakayecheza pambano la kuwania ubingwa wa Afrika baada ya kutwaa ubingwa wa Tanzania katika uzito wa juu.
CCM YAFANYA MAZUNGUMZO NA MJUMBE MAALUM WA UMOJA WA MATAIFA MAKAO MAKUU YA
DODOMA
-
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Ndg. Asha-Rose Migiro,leo tarehe 11
Machi 2026 amefanya mazungumzo jijini Dodoma na Balozi Parfait
Onanga-Anyanga,...
16 hours ago
No comments :
Post a Comment