Raisi wa shirikisho la kandanda Tanzania TFF Leodga Chilla Tenga amevitaka vyama vya soka vya mikoa kutoa maoni dhidi ya ushirikiano wa TFF na ZFA.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari na afisa habari wa TFF Florian Kaijage imesema kwamba Tenga amefikia hatua ya kukusanya maoni kwa viongozi wa mikoa ili kutoa fursa ya kupata uwezekano wa kulimaliza tatizo hilo ambalo sasa linaonekana kukua zaidi.
Raisi wa TFF juma lililopita alizungumza na waandishi wa habari kuelezea kwa kina namna ambavyo TFF imekuwa ikitoa ushirikiano wa karibu na ZFA katika maswala mbali ya maendeleo ya soka.
Tenga aliwataka viongozi wa chama cha soka cha Zanzibar kuwa wa kweli na kuacha kuongea mambo ambayo wanafahamu ukweli wake.
Kwa takribani majuma kadhaa sasa ZFA wamekuwa wakilalamika katika vyombo vya habari kwmaba TFF ndiyo kikwazo katika kufanikisha wao kuwa wanachama wa shirikisho la kandanda Duniani FIFA jambo ambalo TFF imekanusha.
Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na Tenga kwenda kwa vyama vya mikoa imesema TFF itakuwa na kikao na chama cha soka visiwani Zanzibar ZFA tarehe 21 Julai 2009 na moja ya ajenda itakayojadiliwa ni pamoja ushirikishwaji ZFA/Zanzibar katika masuala ya FIFA.
MIMEA VAMIZI NI TISHIO KWA IKOLOJIA YA HIFADHI ZETU, BALOZI POLEPOLE
-
Balozi wa Tanzania nchini Cuba Mhe. Humprey Polepole amesema uwepo wa mimea
vamizi katika maeneo yaliyohifadhiwa inaathiri na kubadilisha ikolojia ya
mae...
1 day ago
No comments :
Post a Comment