Iman Mahugira Madega ni mwenyekiti wa timu hiyo yenye maskani yake jangwani Jijini Dar es salaam amesema taarifa za kambi ya klabu hiyo kwenda Mwanza si za kweli na sasa wataweka kambi katika jengo la klabu hiyo na wanafanya kila jitihada pamoja na uwanja ukamilke haraka ili uweze kutumika katika michezo yao ya ligi kuu.
Madega ameongeza kuwa mpaka sasa zaidi ya shilingi bilioni moja nukta mbili zimekwishatumika ambapo kuna vyumba vya kulala ishirini na tisa ambapo kila chumba watalala wachezaji wawili wawili pamoja na sehemu ya kuogelea swimming pool na sehemu za kupumzikia.
Akizungumzia kuhusu katibu ,mhasibu na msemaji wa kuajiriwa amesema suala hilo lipo kwenye mchakato wa kutafuta watendaji hao kwani wanafahamu kuwa hawataweza kushiriki ligi kuu bila ya kutekeleza agizo hilo la Tff.
No comments :
Post a Comment