Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, October 9, 2012

Mapacha Watatu ndani ya ‘Back in Town’ Mango






Na Elizabeth John

BENDI ya Mapacha Watatu ‘Wakali wa Town’, inatarajiwa kufanya onesho kubwa litakalojulokana kwa jina la ‘Back in Town’, litakalorindima ndani ya ukumbi wa Mango Garden Kinondoni jijini Dar es Salaam, Oktoba 19 mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja wa bendi hiyo, Hamisi Dakota, alisema onesho hilo litakuwa la kwanza jijini, baada ya kuwa kwenye ziara ya Kampuni ya Vadocom, wakitangaza huduma ya M-Pesa mikoa mbalimbali.

“Tumerejea Dar es Salaam hivi karibuni, hivyo mashabiki wetu wasubirie kuona mambo makubwa katika onesho hilo, ambalo natumaini litakuwa la kukata na shoka,” alisema Dakota.

Dakota alisema, katika onesho hilo watasindikizwa na mwimbaji wa taarabu, Isha Mashauzi ‘Jike la Simba’, ambako pia watatumia siku hiyo kuwatambulisha waimbaji, wapiga vyombo na wanenguaji wapya, ambao watajiunga na bendi hiyo.

“Hakuna asiyejua kazi yetu na wala hakuna asiyemjua Isha Mashauzi, mashabiki watarajie burudani safi kutoka kwetu,” alisema.

No comments :

Post a Comment