Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, October 5, 2011

Kamati ya mashindano TFF kujadili Daraja la Kwanza Oktoba 10



Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), litakuwa na kikao na viongozi wa klabu 18 za Ligi Daraja la Kwanza Oktoba 10, mwaka huu.

Msemaji wa TFF, Boniface Wambura, amesema ligi hiyo itakayoanza Oktoba 15, mwaka huu, itashirikisha timu za AFC ya Arusha, Burkina Faso ya Morogoro, Majimaji ya Ruvuma, Mbeya City Council ya Mbeya, Mgambo Shooting ya Tanga, Mlale JKT ya Ruvuma na Morani ya Manyara.

timu nyingine ni Polisi ya Dar es Salaam, Polisi ya Iringa, Polisi ya Morogoro, Polisi ya Tabora, Rhino Rangers ya Tabora, Samaria ya Singida, Small Kids ya Rukwa, Tanzania Prisons ya Mbeya, Temeke United ya Dar es Salaam na Transit Camp ya Dar es Salaam, ambazo zitawekwa katika makundi matatu.

Wambura amesema timu za Majimaji na Small Kids, mpaka sasa hazijalipa ada ya ushiriki ya sh. 200,000 na kwamba, zimetakiwa kulipa ada hiyo kabla ya Oktoba 10, mwaka huu ambayo ndiyo siku ya kupanga ratiba.

No comments :

Post a Comment