Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, October 2, 2011

KAMPUNI YA SIMU TANZANIA TTCL YATOA TAARIFA KWA UMMA



UHAMISHAJI NJIA ZA MAWASILIANO

Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) inapenda kuwafahamisha wananchi na wateja wake kwa ujumla kuwa kwa sasa kuna kazi ya uhamishaji wa njia za mawasiliano kandokando ya barabara mpya ya Bagamoyo ( Mwenge – Tegeta).

Kazi ya kuhamisha njia za mawasiliano ni inafanywa na wakala wa barabara (TANROADS) aliyeingia mkataba namba QTN/AE001/2009/2010/DSM/E/146 na mkandarasi.

Katika mkataba huu, Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) jukumu lake kubwa ni kuelekeza na kushauri njia mpya ya mtandao wa simu utakapopita tofauti na njia za awali.

Tunaomba ieleweke kuwa hadi hapo njia mpya ya simu itakapokamilika ndipo ile ya zamani itaondolewa kuepusha wateja kukosa huduma.

Tayari wakala wa barabara(TANROADS ) amekwishakamilisha awamu ya kwanza ya kuhamisha njia za simu kutoka Mwenge mpaka njia panda ya Africana. Na sasa kazi inaendelea kuanzia njia panda Africana kuelekea Tegeta.

Kwa vile kazi inahusisha njia za mawasiliano zilizopo juu na za chini ya ardhi, kitaalam kazi hii lazima iende sambamba na ujenzi wa barabara mpya kwa kuwa katika ujenzi , mkandarasi wa barabara anajenga njia za kupitisha mawasiliano baada ya kupima kina cha kwenda chini, kwani kina cha barabara kinafahamika tu pale udongo unapokuwa umechimbuliwa na mkandarasi wa barabara.

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

No comments :

Post a Comment