Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, June 1, 2011

Big Sam kocha mypa West Ham

Sam

Sam Allardyce

Sam Alardyce ameteuliwa kuwa meneja wa West Ham baada ya timu hiyo kushuka daraja.

Kocha huyo wa zamani wa Blackburn, Newcastle na Bolton anachukua nafasi ya Avram Grant, ambaye alifukuzwa kazi baada ya West Ham kushuka daraja huku ukiwa umebaki mchezo mmoja katika ligi kuu ya England.

"Ni klabu nzuri na yenye utamaduni mzuri na mashabiki thabiti," amesema Allardyce mwenye umri wa miaka 56.

"Nisingechukua kazi hii, kama nisingedhani tutarudi kucheza ligi kuu moja kwa moja."

Meneja wa muda wa West Ham Kevin Keen, ambaye alisimamia timu hiyo katika mchezo wa mwisho na kufungwa mabao 3-0 na Sunderland, alionesha nia ya kuiongoza klabu hiyo katika ligi daraja la kwanza.

Hata hivyo, Keen hana hana uzoefu wa kuongoza, mbali na kuishughulikia timu ya akiba ya West Ham.

Allardyce anataka kusajili wachezaji kadhaa katika juhudi za kutaka kupanda daraja katika msimu mmoja, na ameahidi kuwa na "mtazamo wa ushindi" kwa wachezaji.

No comments :

Post a Comment