Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, June 1, 2011

Owen kuichezea Man U kwa mwaka mmoja

Owen

Michael Owen


Michael Owen ametia saini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Manchester United.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 ambaye mkataba wake ulikuwa unamalizika, ameonesha nia ya kutaka kuendelea kusalia Old Trafford.

"Nimefurahi kubakia kwa mwaka mmoja zaidi. Nawashukuru wote kwa kunitumia ujumbe," alisema Owen kupitia mtandao wa Twitter.

Karibu msimu wote uliopita Owen alikaa benchi akiwa manchester United, huku Wayne Rooney na Javier Hernandez na Dimitar Berbatov wakipewa kipaumbele zaidi kucheza.

Alikuwa mchezaji wa akiba katika mchezo wa fainali ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Barcelona. Amecheza mechi 17 katika msimu wa 2010/2011 na kufunga mabao matano.

No comments :

Post a Comment