Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, April 7, 2014

112 WAFANIKIWA KUINGIA HATUA YA PILI KATIKA MASHINDANO YA KUSAKA VIPAJI VYA UIGIZAJI TANZANIA LINALOENDELEA KUFANYIKA KATIKA KANDA YA ZIWA MKOANI MWANZA




 Majaji wa Shindano la Kusaka la Vipaji vya Uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents wakijadiliana jambo wakati wa Zoezi la kusaka vipaji vya uigizaji kuingia Hatua ya pili kwa washiriki waliofanikiwa kupita kwenye mchujo.Kulia ni Single Mtambalike (Rich Rich), Ivon Chery (Monalisa) na Roy Sarungi.
Washiriki waliofanikiwa kuingia kwenye hatua ya pili wakifanyiwa usaili kwaajili ya hatua ya pili sasa
Muongozaji wa Mradi wa Shindano la Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents, Bw Stanford Kihole (kulia) akitoa maelekezo kwa washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili katika mashindano ya kusaka vipaji vya uigizaji Tanzania likiwa limeaingia hatua ya pili Mkoani Mwanza
Baadhi ya Washiriki waliofanikiwa Kuingia katika Hatua ya Pili ya Shindano la Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents wakiwa makini kusikiliza maelekezo juu ya hatua ya pili waliofanikiwa kuingia.
 Baadhi ya washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili wakiwa mbele ya majaji kwaajili ya kupewa maelekezo ambapo washiriki watapewa muswada (script) kwaajili ya hatua ya pili ambapo wataingia wawili wawili na kuanza kuonyesha vipaji vyao.
Kikosi Kazi kikiendelea kurekodi matukio yanayoendelea katika Shindano la Kusaka Vipaji Vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents linaloendelea kufanyika Kanda ya Ziwa, Mkoani Mwanza.
 Baadhi ya washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili katika Mashindano ya Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents wakiwa makini katika kupitia muswada (script) waliopewa na majaji ili waweze kusoma na baadae kuingia mbele ya majaji na kuonyesha vipaji vyao kutokana na muswada (script) waliopewa.
Baadhi ya washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili wakifanya mazoezi mara baada ya kupewa muswada (script) na majaji kabla ya kwenda kuonyesha vipaji vyao mbele ya majaji.Picha na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

No comments :

Post a Comment