Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, April 26, 2014

TAIFA STARS YALA KICHAPO CHA 3-0 KUTOKA KWA BURUNDI KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO


FT: TAIFA STARS 0: 3 BURUNDI

Dakika 45` za kipindi cha pili zimeshakatika na kuongezwa dakika 3.
Dakika ya 38 kipindi cha pili, stars wanapata kona na kukosa bao la wazi baada ya kazi nzuri ya Msuva na Omary Nyenje kushindwa kugusa mpira kuutumbukiza wavuni.
Dakika ya 35` kipindi cha pili, Stars wapo nyuma kwa mabao 3-0
Dakika ya 30` kipindi cha pili Burundi wanaongoza kwa mabao 3-0.
Dakika ya 25` kipindi cha pili, Taifa stars wapo nyuma kwa mabao 3-0 dhidi ya Burundi.
Dakika ya 19` kipindi cha pili, Taifa Stars inashindwa kumudu kabisa kasi ya Burundi, lakini Kocha Salum Mayanga amefanya mabadiliko yanayoonekana kuwapa uhai Stars.
Burundi wanaandika bao la tatu kupitia kwa Yusuf Ndikumana.
Amis Tambwe anaifungia Burundi bao la pili kwa shuti kali la chini chini lililomshinda kipa Deo Munish.
Dakika ya 9` kipindi cha pili kona inachongwa kueleka lango la Stars, lakini mabeki wanaokoa.
Didier Kavumbagu anadhihirisha kuwa kasi yake ya kufunga ni ileile.
Wachezaji wa Taifa stars hawana kasi kama wanavyocheza katika klabu zao. Sijui tatizo ni nini hapo uwanja wa Taifa.
Jonas Mkude, Harun Chanongo na Himid Mao wamenyanyuliwa na kuanza kupasha moto misuli.
Dakika ya 4` kipindi cha pili, Burundi bado wanaoongoza kwa bao 1-0.
Almanusura Burundi waandike bao la pili, lakini mpira unaokolewa na Dida na kuwa kona inayoondoshwa na Agrey Moris.
Mpira umeshanza hapa uwanja wa Taifa
Kipindi cha pili kinatarajia kuanza hivi punde, naona waamuzi na wachezaji wa akiba wakiingia uwanjani.
HT: TAIFA STARS 0: 1 BURUNDI
Dakika ya 45` kipindi cha kwanza, Didier Kavumbagu anaifungia Burundi bao la kuongoza.
DDakika ya 40` kipindi cha kwanza bao bila kwa bila.
Mpira umesimama hapa uwanja wa Taifa, kipa wa Stars, Deo Munish akiwa chini akigangwagangwa.
Dakika 31` za kipindi cha kwanza zimeshakatika, hakuna bao kwa timu zote.
Mohamed Seif anaikosesha bao Taifa stars kufuatia krosi ya Saimon Msuva.
Stars wanafanya shambulizi kali, lakini shuti alilopiga Saimon Msuva linakuwa mboga kwa kipa wa Burundi.
Dakika ya 16` kipindi cha kwanza hakuna timu iliyoona lango la mwenzake.
Dakika ya 8` kipindi cha kwanza Burundi wanapata kona,lakini Ramadhan Singano `Messi` anaokoa. 
 Mpira umeshaanza uwanja wa Taifa

TAIFA STRS 0 VS 3  BURUNDI

No comments :

Post a Comment