Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, April 4, 2014

RIDHIWANI KIKWETE AKUTANA NA WAANDISHI WA HABARI,KUZUNGUMZIA MWENENDO WA KAMPENI ZAKE




Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano wake na waandishi hao wakati akizungumzia mwenendo mzima wa Kampeni zake,leo April 4,2014,Nyumbani kwake Msoga.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo Jimbo la Chalinze,Ridhiwani Jakaya Kikwete.

MGOMBEA ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM), Ridhiwani Kikwete, amesema akipata ridhaa ya wananchi, atahakikisha anajenga stendi ya mabasi na soko ili kutoa fursa kwa vijana kupata eneo la kuuzia bidhaa zao.

Ridhiwani amesema nia ni kuhakikisha vijana wanaouza bidhaa za vinywaji na zingine waweze kuwauzia abiria wa mabasi yatakayowekewa masharti ya kuingia stendi.

Akizungumza katika mkutano wake na Waandishi wa habari alipokuwa akielezea mwenendo mzima wa Kampeni zake, Ridhiwani amesema kiu yake ni kuona vijana wanapata masoko ya uhakika ya bidhaa zao.

Amesema atashirikiana na  madiwani wa halmashauri kutafuta eneo nzuri la kujenga stendi na soko hilo litasaidia kuinua jimbo la Chalinze kiuchumi.

“Nimesikia watu wanasema kuhamishwa kwa mizani ya Chalinze , vijana watakosa mahali pa kufanyia biashara zao.Kimsingi mizani si eneo la kufanyia biashara kwanza mabasi yanasimama muda mfupi lakini suluhisho ni stendi,”alisema

Alisema lengo ni kuhakikisha wanatumia fursa ya kuwa njia panda ya mikoa ya Kaskazini na Nyanda za juu Kusini na mikoa ya Kati , kuhakikisha kunakuwa na soko la uhakika.

No comments :

Post a Comment