Mwanamuziki wa miondoko ya ragga muffin Moses Ssali, a.k.a Bebe Cool ameripotiwa kupigwa risasi siku ya jumamosi asubuhi na Polisi.
Hatahivyo Polisi na mwanamuziki huyo ambaye amelazwa chini ya uangalizi maalum.
Akizungumza akiwa amelala kitandani katika Hospitali ya Nsambya, Bebe Cool amekanusha taarifa iliyotolewa kwamba kulikuwa na ugomvi kati yake na Polisi ambaye alimpiga risasi.
Lakini pia amekanusha madai ya kwamba alikutwa akifanya mapenzi na wanawake wawili katika gari katika eneo ambalo hairuhusiwi kupaki, sehemu ambayo Polisi huyo alitaka kuwakamata kufuatia kuegesha gari sehemu ambayo siyo sahihi.
“Polisi amenipiga risasi mara nne. sikuwa na hatia. lakini hili linafanyiwa uchunguzi,” anasema Bebe Cool wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Tukio hilo la shambulio lilitokea nyuma ya Supermarket ya Nakummat muda mchache baada ya mwanamuziki kuondoka katika baa na mgahawa wa Effendy, ambao unatazamana na Centenary Park. Risasi alizopigwa pia zilimpata Polisi David Oluka ambaye amelazwa katika Hospitali ya Mulago Hospital.
Mapema usiku huo, Bebe Cool alikuwa akiperform katika tamasha lililohudhuriwa na mwanamuziki nyota wa Marekani Robert Kelly katika klabu ya usiku ya Silk.
Hata hivyo Weasel wa kundi la Goodlife amedai kwamba Bebe alipigwa risasi baada ya kutaka kupambana na Polisi.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment