Mwanariadha wa zamani wa Kenya wa mbio za kati David Lelei amefariki Dunia katika ajali ya gari huku mwanaariadha mwenzake na bingwa wa zamani wa Dunia wa mbio za mita 10,000 Moses Tanui ameumia vibaya kifuani.
kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwanariadha anayeshikilia rekodi ya Dunia yam bio za marathon Paul Tergat, amesema Lelei, 39 na Tanui, 45, walikuwa wakiendesha gari toka Nairobi wakielekea nyumbani kwao Eldoret hapo jana na kkuligonga kilomita chache nje ya Nakuru, Mji wa nne kwa ukubwa nchini Kenya ikiwa na kilomita za mraba 200 magharibi mwa Nairobi.Tergat amesema walikuwa waktoka katika hafla mjini Nairobi na walikuwa wakisafiri kurudi nyumbani Eldoret wakati ajali ihyo ikitokea.
Akiongea kwa maaseikitiko anakiri kwamba wamempoteza Lelei, lakini Tanui amenusurika na amelazwa Nairobi Hospital.
Lelei alishinda medali ya shaba katika mbio za mita 1,500 mwaka 1999 katika michuano ya All African Games iliyofanyika Johannesburg, mwaka huo huo alimaliza akishika nafasi ya saba katika mbio za Dunia zilizofanyika Seville. Inakumbukwa alimaliza akiwa wa nne katika mbo za mita 800 mwaka 2001 katika michuano ya ndani ya Dunia huko Lisbon.
Tanui alishinda mbio za mita 10,000 na kutwaa ubingwa wa Dunia mwaka 1991 katika michuano iliyofanyika Tokyo. lakini pia alishinda mbio za marathon 1996 na 1998 zilizofanyika Boston.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment