Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, February 7, 2010

SAYORE AIBUKA MSHINDI GOFU ZAIN


Ali Mfuruki akipiga mpira kwelekea shimoni wakati wa mashindano ya kila wiki ya gofu ya Lugalo yanayofanyika kwenye viwanbya vya Gofu Lugalo, Zain inadhamini klabi ya Gofu ya Lugalo ili wasaidie kukuza mchezo wa Gofu nchini.
Mchezaji gofu wa klabu ya Lugalo Kibuna shabani akijiandaa kupiga mpira kwelekea shimoni, wakati wa mashindano ya kila wiki ya gofu ya Lugalo yanayofanyika kwenye viwanja vya Gofu Lugalo, Zain inadhamini klabu ya Gofu ya Lugalo ili wasaidie kukuza mchezo wa Gofu nchini.Generali mstaafu Gideon Sayore ameibuka mshindi wa jumla wa mashindano ya mchezo wa gofu yanayofanyika kila Ijumaa katika viwanja vya gofu vya Lugalo vya Jijini Dar es Salaam kwa udhamini wa kampuni ya simu za mkononi ya Zain.
Sayore amejishindia simu mpya ya mkononi aina ya Zain Phone ambayo ndio ilikuwa zawadi ya juu pamoja na chupa ya wine kutoka Zain baada ya kupata pointi 38.Ofisa Uhusiano wa Klabu ya Gofu ya Lugalo Daudi Helela alisema juzi kwamba jumla ya wachezaji 67 walijitokeza katika mashindano ya Ijumaa iliyopita.
‘’Wachezaji wanajitokeza wengi wiki hadi wiki na klabu sasa inasisimka kila Ijumaa. Tunawachezaji wenye vipaji ambao wanaweza kushirikia hata mashindano ya kimataifa. Hakika tunawashukuru Zain kwa udhamini wa Klabu yetu ya Lugalo.
Zain ina mkataba wa miaka mitatu kudhamini klabu ya gofu ya Lugalo, lengo la Zain ni kusaidia kukuza mchezo wa gofu ili upendwe zaidi nchini kama michezo mingine na imekuwa ikitoa zawadi mbali mbali ikiwemo zawadi kubwa kama simu za aina ya Blackberry ili kuwavutia wachezaji.

No comments :

Post a Comment