Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, February 10, 2010

SIMBA YATAKIWA KUFANYA UCHAGUZI KABLA YA MECHI 3

KAMATI ya Michezo ya Wilaya ya Ilala, imeiagiza klabu ya Simba ifanye uchaguzi wake mkuu ndani ya Machi 3 mwaka huu, vinginevyo Serikali itaingilia kati.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam Mwenyekiti wa kamati hiyo, Prisca Kissila amesema, Kamati ya Michezo inauagiza uongozi wa klabu hiyo uhakikishe lazima unafanya uchaguzi ndani ya siku 90 kutoka Desemba 3 mwaka jana.
Amesema kwa hiyo watalazimka kufanya uchaguzi kabla ya Machi 3 mwaka huu, sera ya maendeleo ya michezo inawalazimisha kifungu namba sita lazima waheshimu kipindi cha uongozi.
Kissila amesema , katika kikao walichokaa juzi (jana) maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya kwa Kamati hiyo yafuate katiba ya Simba pamoja na sheria namba 12 ya mwaka 1967 na marekebisho yake namba 6 mwaka 1971 ya Baraza la Michezo la Taifa na kanuni za usajili namba 442 za mwaka 1999.
Aidha ameongeza kwamba uongozi wa Simba uliomaliza muda wake, ulitakiwa kuitisha mkutano simu 30 kabla ya kumaliza kipindi cha uongozi au baada ya siku 30, lakini uongozi haukufanya hivyo.
Kissila amesema, uongozi wa Simba umekiuka katiba ya chama chao pamoja na kanuni za Baraza la Michezo la Taifa, uliitisha mkutano mkuu ndani ya siku 46.
Aidha amesema muhtasari wa kikao haukuletwa kwa msajili tangu wamalize kikao chao, katiba yao inasema Kamati ya Utendaji itapanga tarehe ya Uchaguzi Mkuu na si Mkutano Mkuu, lakini uongozi wa Simba ulidai mkutano utapanga tarehe ya uchaguzi ni kinyume na katiba yenye ridhaa yao.
Hata hivyo kabla ya ofisi ya msajili haijatoa ufafanuzi kundi la baadhi ya wanachama wa Simba wakiongozana na aliyekuwa katibu Mwenezi, Said Rubeya 'Seydou' lilivamia ofisi ya msajili huyo huku wakiwasonga viongozi waliowakuta kwa kuwalalamikia kuwa ndio wanaokwamisha uchaguzi.
Hata hivyo Kissila amesema, viongozi wa Simba jana waliitwa na Mkuu wa Wilaya lakini wamekaidi agizo hilo, hivyo Mkuu huyo ameahidi kuwatafuta ili waweze kutoa tamko la terehe ya uchaguzi kama walivyoamuliwa.

No comments :

Post a Comment