Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, February 1, 2010

BEYONCE:MALIKIA MPYA WA GRAMMY AWARDS

Tuzo maarufu za muziki za Grammy zimemalizika muda mfupi uliopita jijini Los Angeles.Kama kawaida ya tuzo maarufu kama hizo,huwa kuna kuvunjwa kwa rekodi au kuwekwa rekodi mpya,vituko mbalimbali, mavazi ya kukumbukwa na pia performances za kukumbukwa.
Kwa mwaka huu,rekodi mpya imewekwa na Beyonce Knowles.Binti huyo ambaye ni mke wa rapper maarufu ulimwenguni,Jay-Z ameibuka na jumla ya tuzo sita na hivyo kuweka rekodi ya kuwa mwanamuziki wa kike wa kwanza kushinda idadi hiyo ya tuzo katika usiku mmoja wa tuzo za Grammy!
Kwa upande wa performances ambazo nitazikumbuka kwa muda ni pamoja na performance aliyofanya Pink huku akijibinubinua hewani kwa kutumia kipande cha nguo! Kuna haja ya kuchunguza zaidi ili kujua kiasi gani cha ile performance ni kweli na kiasi gani ni uzushi.It was hot though.
Nyingine niliyoipenda ni performance ya Lil Wayne(yuko mbioni kwenda jela kwa miezi nane na huenda hii ilikuwa ni performance yake ya mwisho), Drake na Eminem. Nilifurahi kumuona Eminem akiwa bado yupo fit na huku uwezo wake wa kumiliki jukwaa ukiwa pale pale.Hapo katikati alipotea kutokana na matumizi ya kutisha ya madawa ya kulevya.
Mavazi: Mimi sio mtaalam sana wa mambo ya mavazi.Lakini hata hivyo hiyo haikunizuia kuona kwamba Lady Gaga alitia fora kwa kivazi alichovaa baada ya ku-perform na kuungana na wenzake katika audience.Sijui bado jina la kitu alichovaa;ni gauni au?
Kwa ujumla tuzo kubwa kubwa zilienda kama ifuatavyo;

* Record of the Year – Kings of Leon – “Use Somebody”
* Album of the Year – Taylor Swift – ‘Fearless’
* Song of the Year – Beyonce – “Single Ladies (Put a Ring On It)”
* Best New Artist – Zac Brown Band
* Best Female Pop Vocal – Beyonce – “Halo”
* Best Male Pop Vocal – Jason Mraz – “Make It Mine”
* Best Duo or Group With Vocals – Black Eyed Peas – “I Gotta Feeling”
* Best Pop Vocal Album – Black Eyed Peas – ‘The E.N.D

No comments :

Post a Comment