Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, February 9, 2010

RONALDINHO ATEMWA TIMU YA TAIFA BRAZILI

Mchezaji Ronaldinho huenda akaikosa michuano ya soka Dunia baada ya kuachwa katika kikosi cha Taifa cha Brazili ambacho kinajiandaa na michezo ya kirafikki ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea Afrika Kusini.
Ataukosa mchezo utakaopigwa katika dimba la Emirates dhidi ya timu ya taifa ya Ireland utakaopigwa Machi 2.
Nyota huyo anayeichezea klabu ya AC Milan hajaichezea timu ya taifa ya Brazil tangu kuanza kwa mwaka 2009, lakini kwa sasa ameonekana kuimarika zaidi huku mashabiki wa soka wa Brazili wakishinikiza aitwe katika timu ya taifa.
Lakini kocha Dunga amekataa kufuata msukumo wa mashabiki pamoja na vyombo vya habari kumuita nyota huyo wa zamani wa Barcelona.
Dunga ambaye alikuwa kapteni katika kikosi cha Brazili kilichotwaa uchampion wa Dunia mwaka 1994 ameendelea kuwa waamini kina Michel Bastos (Lyon), Juan na Doni ambao wote wanacheza soka katika klabu ya AS Roma, Kleberson (Flamengo) na Gilberto (Cruzeiro).
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester City Robinho, ambaye anacheza kwa mkopo katika klabu ya Santos, amejumuishwa katika kikosi cha taifa pamoja na kiungo wa Liverpool Lucas. lakini hakuna nafasi kwa kiungo wa Manchester United Anderson.
Ronaldinho alikuwa mmoja wa wachezaji waliyokiwezesha kikosi cha Brazili kutwaa uchampion wa Dunia mwaka 2002 na ndiye aliyeitoa England katika michuano hiyo baada ya kumdanganya golikipa David Seaman kwa shuti la mpira uliyokufa.
Mkongwe wa soka wa Brazil Pele ni mmoja wa watu ambao waliomba Ronaldinho ajuimuishwe katika kikosi kitakachotinga katika fainali za Dunia.
Ronaldhinho amejitokeza mara 87 katika timu ya taifa ya Brazili, akifunga jumla ya magoli 32.
Lakini pia amefanikiwa kutajwa mara mbili kuwa mwanasoka bora wa Dunia mwaka 2004 na 2005 na amefanikiwa kutwaa tuzo ya Ballon d'Or ama (european player of the year) mara moja.
________________________________________
Brazil squad to face Ireland:
Goalkeepers: Julio Cesar (Inter Milan), Doni (Roma).
Defenders: Maicon (Inter Milan), Daniel Alves (Barcelona), Gilberto (Cruzeiro), Michel Bastos (Lyon), Juan (Roma), Lucio (Inter Milan), Luisao (Benfica), Thiago Silva (AC Milan).
Midfielders: Gilberto Silva (Panathinaikos), Josue (Wolfsburg), Felipe Melo (Juventus), Lucas (Liverpool), Kaka (Real Madrid), Ramires (Benfica), Elano (Galatasaray), Julio Baptista (Roma), Kleberson (Flamengo).
Forwards: Robinho (Santos), Adriano (Flamengo), Nilmar (Villarreal), Luis Fabiano (Seville).

No comments :

Post a Comment