Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, February 3, 2010

TID NA CHIDI BENZI NDANI YA NGOMA MOJA

Yapo majina ya wasanii wa kizazi kipya ambao ukisikia wameshirikiana(collaborate)kutengeneza kazi fulani, basi unakuwa na imani kubwa kwamba kazi hiyo ina nafasi kubwa ya kuwa nzuri. Hiyo inatokana na uzoefu na pia zingatio za kazi zao zilizopita,nafasi waliyonayo katika uwanja mpana wa sanaa ya muziki na mambo kama hayo.
Hivi karibuni nilipoletewa kazi mpya na kuambiwa kwamba wasanii waliomo katika kazi hiyo ni TID(Top in Dar) na Chid Benz, nilikuwa na uhakika kwamba kazi hiyo itakuwa imesimama.TID na Chid ni miongoni mwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao binafsi nawaheshimu na sioni noma kusema kwamba nazipenda nyingi kati ya kazi zao.Habari nzuri ni kwamba hawakuniangusha katika kazi hii ya hivi karibuni inayokwenda kwa jina Huyu.
Kama zilivyo kazi nyingi za wasanii wetu siku hizi,hii pia ni hadithi ya mapenzi (bado natamani wigo wa yaliyomo(content) za kazi za wasanii upanuke zaidi na kugusa maeneo mengine yanayoizunguka jamii).Kinachoufanya wimbo huu uwe tofauti ni uwezo binafsi wa wasanii husika na hadithi yenyewe.
Kazi hii imepikwa pale Tetemesha Records(kule kule alikoibukia Hussein Machozi) chini ya George Mpanda au maarufu kama Kid Bwoy.

No comments :

Post a Comment