Serikali ya Togo imekasirishwa na kitendo cha kufungiwa na shirikisho la soka barani Afrika kwa miaka minne imetishia kuwashukulia hatua zaidi za kisheria.
"Haya ni maamuzi ya kushitukiza sana nah ii inamaanisha hawa watu yaani (Caf) hawana uchungu wowote na maisha ya binaadamu," Anasema waziri wa mambo ya ndani wa Togo Pascal Bodjona.
Ameongeza kuwa hatua hiyo ni dharau kwa taifa la Togo na familia za wale ambao ndugu zao walipoteza maisha pamoja na wote waliyoathirika na shambulio hilo.
Amesema wanasubiri taarifa rasmi ndipo watachukua hatua za kisheria kutatua tatizo hilo.
Shirikisho la kandanda Dunia limekataa kuzungumza chochote dhidi ya hatua ya kufungiwa Togo.
Taarifa ya Caf ilikuwa ikisema: "kamati ya utendaji imeifungia Togo kutoshiriki fainali mbili za mataifa ya Afrika na kukitoza chama cha soka cha nchi hiyo kiasi cha Dola za marekani 50,000."
Kocha msaidizai wa timu ya taifa ya Togo na Afisa habari walipoteza maisha wakati basi lao liliposhambuliwa mjini Cabinda Januari 8 walipoteza maisha na serikali kulazimika kuirudisha timu ya taifa nyumbani kwa ajili ya maombolezo ya siku tatu.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment