Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, February 1, 2010

SERIKALI YA TOGO - KUFUNGIWA NI KUDHARAU TAIFA

Serikali ya Togo imekasirishwa na kitendo cha kufungiwa na shirikisho la soka barani Afrika kwa miaka minne imetishia kuwashukulia hatua zaidi za kisheria.
"Haya ni maamuzi ya kushitukiza sana nah ii inamaanisha hawa watu yaani (Caf) hawana uchungu wowote na maisha ya binaadamu," Anasema waziri wa mambo ya ndani wa Togo Pascal Bodjona.
Ameongeza kuwa hatua hiyo ni dharau kwa taifa la Togo na familia za wale ambao ndugu zao walipoteza maisha pamoja na wote waliyoathirika na shambulio hilo.
Amesema wanasubiri taarifa rasmi ndipo watachukua hatua za kisheria kutatua tatizo hilo.
Shirikisho la kandanda Dunia limekataa kuzungumza chochote dhidi ya hatua ya kufungiwa Togo.
Taarifa ya Caf ilikuwa ikisema: "kamati ya utendaji imeifungia Togo kutoshiriki fainali mbili za mataifa ya Afrika na kukitoza chama cha soka cha nchi hiyo kiasi cha Dola za marekani 50,000."
Kocha msaidizai wa timu ya taifa ya Togo na Afisa habari walipoteza maisha wakati basi lao liliposhambuliwa mjini Cabinda Januari 8 walipoteza maisha na serikali kulazimika kuirudisha timu ya taifa nyumbani kwa ajili ya maombolezo ya siku tatu.

No comments :

Post a Comment