Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, February 26, 2010

KICKBOXING LIGI KUANZA JUMAMOSI

Japfet Kaseba mwenye T-shirt ya njano akiwa na wapiganaji wengine wa mchezo kick Boxing walipozuru Radio Times FM, mwenye karatasi mi mdau wa viwanjani Amri Massare.
Zaidi ya mabondia nane leo wamepima uzito pamoja na Afya zao tayari kupambana katika ligi ya mchezo huo itakayoanza siku ya jumamosi majira ya saa kumi katika ukumbi wa DDC Magomeni jijini Dar es Salaam.
Mwandaji wa ligi hiyo ambaye ni bingwa wa dunia wa mchezo huo Japhet Kaseba amesema kwamba sambamba na upimaji wa mabondia wametoa mafunzo na semina kwa waalimu na waandishi habari.
Japhet Kaseba amesema maandalizi yote yapo tayari na kiingilio ni Tshs 4000 kwa VIP na kawaida 2000.
Aidha kaseba amewataka watanzania kujitokeza kwa wingi katika mashindano hayo ya mchezo wa kick Boxing ambayo yanafanyika nchini Tanzania kwa mara ya kwanza.
Amesema anaamini itakuwa ni Burudani ya pekee kushuhudia vijana wenye vipaji lakini hawakuwahi kupewa nafasi ya kuonyesha uwezo wao kutokana na mapromota uchwara ambao wamekuwa na tabia ya kutaka wapiganaji wenye majina kwa kutaka faida kubwa, na kuwasahau wengine ambao wanavipaji lakini hawana majina.

No comments :

Post a Comment