Japfet Kaseba mwenye T-shirt ya njano akiwa na wapiganaji wengine wa mchezo kick Boxing walipozuru Radio Times FM, mwenye karatasi mi mdau wa viwanjani Amri Massare.
Zaidi ya mabondia nane leo wamepima uzito pamoja na Afya zao tayari kupambana katika ligi ya mchezo huo itakayoanza siku ya jumamosi majira ya saa kumi katika ukumbi wa DDC Magomeni jijini Dar es Salaam.
Mwandaji wa ligi hiyo ambaye ni bingwa wa dunia wa mchezo huo Japhet Kaseba amesema kwamba sambamba na upimaji wa mabondia wametoa mafunzo na semina kwa waalimu na waandishi habari.
Japhet Kaseba amesema maandalizi yote yapo tayari na kiingilio ni Tshs 4000 kwa VIP na kawaida 2000.
Aidha kaseba amewataka watanzania kujitokeza kwa wingi katika mashindano hayo ya mchezo wa kick Boxing ambayo yanafanyika nchini Tanzania kwa mara ya kwanza.
Amesema anaamini itakuwa ni Burudani ya pekee kushuhudia vijana wenye vipaji lakini hawakuwahi kupewa nafasi ya kuonyesha uwezo wao kutokana na mapromota uchwara ambao wamekuwa na tabia ya kutaka wapiganaji wenye majina kwa kutaka faida kubwa, na kuwasahau wengine ambao wanavipaji lakini hawana majina.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment