Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, February 11, 2010

NGUZA MBANGO NA FRANCIS NGUZA WAACHIWA HURU, VIKING NA PAPII NGUZA WARUDI JELA!!

Maofisa Magereza wakiwasindikiza washtakiwa wa familia moja wa kosa la kulawiti watoto,kuingia katika Mahakama ya Rufaa Dar es Salaam leo asubuhi. kuanzia kushoto ni Nguza Vickig na wanawe Papy Nguza,Nguza Mbangu,Francis Nguza.
Familia ya Mwanamuziki Nguza Viking imemuomba Raisi Jakaya Kikwete kuingilia kati suala la kuendelea kukaa gerezani kwa mwanamuziki huyo na mwanaye JohnSon Nguza maarufu Papii Kocha.
Ombi hilo limetolewa leo na shangazi wa nguza viking, bibi Mwisha Matuka Bizoo, baada ya mahaka ya Rufaa kuwaachia huru, watoto wao, Francis Nguza na Nguza Mbangu na kumrejesha Gerezani mwanamuziki huyo na mwanawe Papii Kocha.
Nguza Viking, na watoto wake watatu walihukumiwa kifungo cha maisha Jela mwaka 2004 na mahaka ya hakimu mkazi kisutu Jijini Dar es Salaam baad ya kupatikana na hatia ya kuwadhalilisha kijinsia waoto wa kike eneo la sinza jijini.Nguza na mwanae Papii Kocha wakirejeshwa lupango kutumikia kifungo cha maisha.
Hata hivyo, baada ya hukumu iyo kupitiwa upya na majaji wa tatu, Bwana Salum masati, Bwana Mbaruk Mbaruk, wakiongozwa na Bwana Nathalia Kimaro, makama hiyo imebaini kuwa watoto wawili wa Nguza Viking, Fransis Nguza na Nguza Mbangu walifungwa kimakosa.
Akisoma huku hiyo, Jaji Neema Chusi, amesema wakati makosa hayo yakifanyika jijini Dar es Salaam, Nguza Mbangu, alikuwa kwenye ziara za kimuziki, na Fransis Nguza, alikuwa Shuleni.

No comments :

Post a Comment